Diamond ndani tuzo za BET awards 2016
Posted in
afrika mashariki
,
Burudani
No comments
Friday, May 20, 2016
By
danielmjema.blogspot.com
Kazi imeanza tena, yule mkali wa kuwanyoosha kwenye tuzo mbali mbali, ametueliwa tena kuwania tuzo ya BET awards 2016. Msanii wa Bongo fleva anayendelea kukimbiza na kuitangaza muziki wa Afrika Mashariki, Diamond Platnumz kutoka Tanzania ametueliwa kuwania tuzo hiyo pamoja na mastaa wengine wakubwa akiwemo Rihanna na Beyonce.
Diamond amekuwa msanii pekee kutoka Afrika Mashariki kutajwa kuwani tuzo hiyo ambapo ameingia katika kipengele cha Msanii Bora wa Kimataifa toka Africa.
Diamond ameshukuru kwa kuchaguliwa kuwania tuzo kwenye kipengele cha Best international Act Africa ambapo ameyaandika maneno haya baada ya kufikiwa na taarifa "Ningependa niwashukuru kwa Sapoti kubwa Manayozidi kunipa na niwajuze kuwa kijana wenu nimechaguli kuwania tunzo ya Msanii Bora wa Kimataifa toka Africa kwenye tunzo za BET #BETAwards America"
Tuzo za BET 2016 ambazo zitatolewa nchini Marekani zimeanza kuchukua nafasi kwenye headlines baada ya kutangazwa list ya waliochaguliwa kuwania tuzo hiyo huku Beyonce, Rihanna na Drake wakitangazwa kuongoza kwa kuwania tuzo zaidi ya moja.
Habari Zingine
- Wachimbaji mgodi 15 waliokwama ardhini waokolewa nchini Tanzania
- Al-Shabab washambulia kambi ya majeshi ya Kenya nchini Somalia
- RAPPER WA CAMEROON, NGOMA AACHIA VIDEO YA WIMBO MPYA ‘ALL LES DAY’, AIELEZEA COLLABO YAKE NA RAY VANNY
- New Hit: Lady Jay Dee – Sawa Na Wao
- Madonna atembelea makazi duni ya Kibera, Nairobi
- Timbulo: SIjarejea kwenye ualimu
- Vijana wazidi kujitokeza usaili wa Maisha Plus East Africa, Dar es salaam yatia fora
- UHURU WA HABARI SIO KUIANGALIA TU SERIKALI - MWAKYEMBE
- JUKWAA LA WAHARIRI TANZANIA LATANGAZA KUSUSIA KUANDIKA HABARI ZA MKUU WA MKOA WA DAR
- WENGI WALIVYOJITOKEZA KUMUAGA MWANA TBN JENNIFER LIVIGHA (CHINGA ONE) HOSPITALI YA AMANA JIJINI DAR
Mjulishe Mwenzako
0 MAOINI :