Fainali ya tano, Poland haijawahi kuifunga Ujerumani

Posted in
No comments
Friday, June 17, 2016 By danielmjema.blogspot.com

Michuano ya Euro 2016 imeendelea kama kawaida June 16 2016, michuano inazidi kuwa migumu kutokana na timu kuingia katika round ya pili ya hatua ya Makundi, hivyo zinahitaji point ili kujiweka katika nafasi nzuri zaidi, June 16 imechezwa michezo mitatu, lakini mchezo kati ya Ujerumani dhidi ya Poland ulionekana kuwa mgumu zaidi.
Katika mchezo wa Ujerumani dhidi ya Poland umemalizika kwa timu hizo kutoka sare ya 0-0, hivyo kutokana na timu hizo michezo yao ya kwanza ilipata ushindi, zote zinakuwa zimetimiza point nne ila Ujerumani anaongoza Kundi C kwa tofauti ya magoli, wakati Ukraine kutokana na kutokuwa na point hata moja, wanasubiri kukamilisha ratiba.
qwerty
Baada ya matokeo hayo hii inakuwa fainali ya tano kubwa kwa timu ya taifa ya Poland kushindwa kupata ushindi mbele ya timu ya taifa ya Ujerumani, Mario Gotze na Mesut Ozil walionekana kupata nafasi amabazo wangeweza kuipatia ushindi Ujerumani, ila golikipa wa Poland Lukasz Fabianski alionekana kuwa imara kwa kuokoa hatari zote golini.

Habari Zingine

0 MAOINI :

Fadhili Athumani



EastAfrica Swahili Blogger, Journalist at Mwanaspoti Kenya, Nairobi Kenya, Call: +254705246475, whatsapp:+255654724337, Email: fadhiliathumani85@gmail.com

Proudly Powered by EAMG .