Serikali Kuleta Madaktari Kutoka Nje Ya Nchi - Bilioni 200 Zatengwa Kuwalipa-mbona sielewi hii filamu hivi muongozaji na mtunzi ni nani au ni ya kanumba?.
                      Posted in 
                      
                            No comments
                          
Sunday, July 1, 2012
                      By 
                      danielmjema.blogspot.com
Serikali
 imeamua kuagiza madaktari kutoka nchi za nje watakaochukua nafasi ya 
wale wa hapa nchini ambao wamegoma kuanzia mwishoni mwa wiki iliyopita.
Habari
 kutoka katika moja ya vyanzo vya kuaminika zimesema kuwa uamuzi huo wa 
serikali ulipitishwa katika kikao cha Baraza la Mawaziri kilichokutana 
mjini Dodoma juzi chini ya uenyekiti wa Rais Jakaya Kikwete.
Habari
 kutoka ndani ya kikao hicho zilidai kuwa Rais Kikwete alikerwa na tabia
 ya madaktari kupingana na serikali licha ya juhudi zote zilizofanywa 
kuboresha maslahi yao.
Kwa
 mujibu wa habari hizo, kiasi cha sh bilioni 200 kimetengwa kwa ajili ya
 kuwaleta na kuwagharimia  madaktari hao wa nje na pia baraza 
limepitisha azimio la kuzungumza na hospitali za jeshi kama  Lugalo na 
zingine ndogo kubeba jukumu hilo kwa sasa pamoja kuagiza madaktari 
wastaafu wote warejee kazini katika kipindi hiki cha mgomo.
Habari
 zimedai kuwa madaktari hao wanasadikiwa watatoka katika nchi rafiki, 
zikiwemo India, China, Cuba na Afrika Kusini, na kwamba wataziba 
kikamilifu pengo la wale wa hapa nchini ambao wamegoma.
Inaelezwa
 kuwa mara baada aya kukamilika na kuanza rasmi kwa huduma za matibabu, 
madaktari wa hapa nchini waliomo katika mgomo na wale zaidi ya 200 
waliodaiwa kufukuzwa na serikali kimyakimya, watalazimika kurejeshwa 
kazini kwa masharti makali.
Hata hivyo, uamuzi wa serikali  kuwatimua madaktari wakati suala lao liko mahakamani, umewagawa wabunge.
Baadhi
 ya wabunge walijaribu kuhoji suala hilo Bungeni, lakini walikwama baada
 ya Spika Anna Makinda  kuzuia mjadala huo kwa madai kuwa suala hilo 
liko mahakamani.
Mbunge
 wa Nzega, Dkt. Hamis Kigwangala, alisema kuwa kilichofanywa na serikali
 ni kiini macho kwani juzi Waziri Mkuu Mizengo Pinda  alisema serikali  
haiwezi kutoa kauli dhidi ya madaktari kwa madai kuwa kuna kesi 
mahakamani, “Juzi serikali imesema kuwa haiwezi kutoa kauli kwa vile 
jambo hilo lipo mahakamani, sasa imewezaje kuwafukuza madaktari wakati 
jambo lipo mahakamani?” alihoji Dkt. Kigwangala.
Aliitaka serikali kuondoa kesi hiyo ili kurejesha majadiliano kwani ndio njia pekee ya kukabiliana na mgogoro huo.
Mbunge
 wa Ubungo, John Mnyika, alimshangaa Spika Anna Makinda kuzuia mjadala 
huo kwani ungeweza kujadiliwa bila kuingilia uhuru wa mahakama.
Juzi
 uongozi wa Hospitali ya Taifa Muhimbili,  uliwafukuza kazi madaktari 
229 walioko katika mafunzo kwa njia ya vitendo kutokana na mgomo 
unaoendelea wa kushinikiza  kulipwa posho zao za mwezi mmoja.
Hospitali zingine ambako madaktari wamefukuzwa kutokana na mgomo huo ni pamoja na Mbeya na Dodoma.
Habari Zingine
Mjulishe Mwenzako
 
 
 
 


 
 
0 MAOINI :