SHIGONGO AELEZEA SABABU ZA KUSHIKILIA PASSPORT YA JOSE CHAMELEONE.

Posted in
No comments
Sunday, July 29, 2012 By danielmjema.blogspot.com



  Jose Chameleone na watu wake kwenye maandamano ulipo ubalozi wa Tanzania Uganda.
Najua watu wengi wametaka kusikia Mr Eric Shigongo C.E.O wa Global Publishers atazungumza nini kuhusu kuishikilia passport ya mwimbaji Jose Chameleone wa Uganda.
Kama bado hujaisikia hii ishu, inabidi ufahamu kwamba kuna ishu inaendelea kati ya watu hao wawili, Big Boss Eric Shigongo anamdai Chameleone dola elfu 3500 ambazo alilipwa mwanzoni kabla ya kulipwa dola elfu 8 baadae kwa ajili ya kuja kuperfom Tanzania kwenye Tamasha la usiku wa matumaini Uwanja wa taifa.
Kwenye mkutano na waandishi wa habari jana.
Alikuja kupiga show vizuri kwa mujibu wa mkataba wa pili aliolipwa dola elfu 8 lakini baada yakumaliza show, kesho kutwa yake ndio stori ikatoka kwamba Jose Chameleone kanyang’anywa Passport na Shigongo kwa sababu anamdai dola elfu tatu mia tano za mwanzo.
Chameleone alisaidiwa kurudi kwao na ubalozi wa Uganda Tanzania lakini anachosema kuhusu kunyang’anywa passport ni kwamba hizo pesa hakulipwa yeye bali promota feki aitwae George huko Kampala Uganda, so Chameleone aliporudi home alimkamata George na kumepeleka polisi lakini baadae aliachiwa huru.
Juzi Jose Chameleone aliandamana na watu wake mpaka ubalozi wa Tanzania Uganda akiutaka ubalozi huo ufanye juu chini apate passport yake anayodai kanyang’anywa na Eric Shigongo kwa sababu anamdai.
Kabla ya hii ishu kuwa kubwa, tayari Global Publishers ambao ni waandaaji walishafanya maamuzi mengine ya busara ya kwenda kwenye Ubalozi wa Uganda hapa Tanzania na kueleza kilichotokea lakini hawakupata msaada wowote na baadhi ya wafanyakazi wa ubalozi huo walimfanya mwakilishi wa Global Publishers kupata picha ya fikra mbaya baada ya wafanyakazi hao wawili kuongea kwa kiganda huku wakicheka baada ya kupewa hiyo taarifa ya Chameleone kutapeli.
Erick Shigongo amesema “mimi sisemi kwamba Watanzania tuwe watu wabaya lakini ni vizuri tukajua jinsi ya kusimamia haki zetu, sisi tumelelewa kwa upole toka wazee wetu huko nyumba tunarithi tu hiyo kitu”
.
Kuhusu huyo Promota feki aitwae George, Shigongo amesema “mimi nilimfahamu George kupitia kwa Kidumu alieniambia ni mtu pekee anaefanya kazi na wasanii wengi Uganda, Kidumu alipokwenda Kampala walikutana hawa watu Chameleone akiwa ana haraka haraka ya kuondoka kwenda kwenye show Sudan, hivyo mbele ya Kidumu Chameleone akaruhusu huo mkataba usainiwe na George huku Kidumu ndio akitoa hizo pesa”
Juzi Chameleone alipoandamana alikua na mabango mbalimbali huku mengine yakiandikwa Erick Shigongo yuko juu ya sheria kiasi gani mpaka kuishikilia passport yake toka july 9 2012.
Kuhusu ishu ya kuishikilia Passport ya Chameleone, Shigongo amesema “hakuna mtu anaeshikilia Passport ya Chameleone isipokua Chameleone alifata utaratibu wa kawaida kwenye hoteli anapoingia kwa kukabidhi fedha zake na document muhimu na Hoteli ilikua ni ya kwetu, tulipoanza kumdai tukitaka atulipe kabla mazungumzo hayajafika mwisho wakati wa mvutano akaondoka bila kuaga hotelini, hakunyang’anywa passport yake ila aliziacha Reception”
.
Kuhusu kumchukulia hatua za kisheria, Shigongo amesema “kuna mambo mawili yatafanyika kwa sababu nilipokutana na uongozi wa Wizara ya mambo ya nchi za nje waliniomba nirudishe Passport ili watumie njia za kidiplomasia kuhakikisha nalipwa pesa zangu, hiyo ni option ya kwanza… ya pili tunawasiliana na wanasheria wetu ili kuona namna gani tunaweza kushughulikia hili swala”

Habari Zingine

0 MAOINI :

Fadhili Athumani



EastAfrica Swahili Blogger, Journalist at Mwanaspoti Kenya, Nairobi Kenya, Call: +254705246475, whatsapp:+255654724337, Email: fadhiliathumani85@gmail.com

Proudly Powered by EAMG .