Moses Sithole: Handsome aliyetikisa kwa mauaji ya kutisha ya wanawake 38….!
Posted in
No comments
Monday, June 17, 2013
By
danielmjema.blogspot.com
Dk. Mervyn MansellMmoja wa wahanga wake
Moses Sithole
Mnamo Septemba 17, 1995, Dk. Mervyn Mansell aliombwa na Polisi ili
kusaidia kujua tarehe ya kifo cha mwili wa mtu uliyookotwa katika pori
lililoko katika eneo la machimbo ya madini la Van Dyke eneo ambalo lipo
jirani na mji wa Boksburg nchini Afrika ya kusini. Dk. Mansell mtaalamu
wa elimu ya wadudu akifanya kazi katika kitengo cha utafiti wa kilimo
katika halimashauri ya jiji la Pretoria alikuwa amepata taarifa hizo
wiki mbili mapema kutoka kwa askari wa upelelezi aitwae Vivian Bieldt.
Askari huyo alikuwa amesoma utafiti fulani kuhusiana na funza kutumika kukadiria siku kifo kilipotokea kwa usahihi kabisa pale inapotokea mwili wa mtu aliyeuawa na kutekelezwa mahali na kuonekana baada ya siku kadhaa ukiwa umeshaanza kuharibika kwa kushambuliwa na funza.
Askari huyo alikuwa amesoma utafiti fulani kuhusiana na funza kutumika kukadiria siku kifo kilipotokea kwa usahihi kabisa pale inapotokea mwili wa mtu aliyeuawa na kutekelezwa mahali na kuonekana baada ya siku kadhaa ukiwa umeshaanza kuharibika kwa kushambuliwa na funza.
Siku
hiyo hiyo baadae Inspekta Bieldt alimpigia tena simu Dk. Mansell na
kumjulisha kwamba, sio mwili wa mtu mmoja tena bali wamegundua miili ya
watu watano. Kwa upande wa Dk. Mansell hii ilikuwa ni kesi ya kwanza
nchini humo kuwahusisha wataalamu wa elimu ya wadudu katika upelelezi.
Hata hivyo jambo la kushangaza ni kwamba mpaka siku ya pili wakiendelea
kufanya upelelezi katika eneo hilo, walipata jumla ya miili watu kumi
wote wakiwa ni wanawake. Hiyo ilionyesha kwamba muuaji alikuwa akiuwa na
kufika pale kuitelekza miili ya watu aliowauwa katika eneo hilo.
Mwili
wa kwanza uligunduliwa siku ya Jumamosi jioni ya Septemba 16 1995,
wakati Polisi mmoja alipotoka na mbwa wake kwenda kuwinda sungura katika
pori hilo. Zaidi ya Polisi 30 wakiwemo askari wa upelelezi kutoka
katika kitengo cha upelelezi wa kesi za mauaji na unyang’anyi wa kutumia
silaha cha East Rand waliwasili katika eneo hilo, pia walikuwepo
wataalamu wa kukusanya ushahidi kitaalamu ambao walikuwa na jukumu kubwa
la kuchunguza eneo la tukio ili kukusanya ushahidi kwa siku kadhaa.
Si
hivyo tu, bali pia Helikopta na mbwa wa Polisi vilihusishwa ili
kuchunguza iwapo kulikuwa na miili mingine iliyotelekezwa katika eneo
hilo.Micki
Pistorius Polisi na mwanasaikolojia alikuwepo pia katika eneo hilo.
Akizungumzia hali aliyokutana nayo katika eneo hilo, alisema kwamba hali
ilikuwa ni ya kutisha sana na hajawahi kukutana na hali hiyo tangu
kuzaliwa kwake.
“Haya
ni moja ya mauaji ya kutisha ambayo sijapata kuyashuhudia katika maisha
yangu, miili ya watu waliouawa ilikuwa imetapakaa kila mahali huku
mingine ikiwa imekaribiana kwa umbali wa mita kadhaa kutoka ulipo mwili
mwingine. Funza walikuwa ni wengi katika eneo hilo kiasi cha kutupanda
katika nguo zetu.” Alisema mama huyo, Polisi na mwanasaikolojia.
Kuna
uwezekano kwamba baadhi ya wanawake wale waliouawa katika eneo hilo na
kutelekezwa mahali hapo. Ilikuwa ni vigumu kuamini kwamba muuaji alikuwa
akiwachukua wahanga wake na kuwapeleka katika eneo hilo ambapo kulikuwa
na miili ya watu waliuawa na muuaji huyo tena ikiwa tayari imeshaanza
kuharibika ili kuwatisha na kuwajengea hofu kabla ya kuwabaka kuwauwa na
kutelekeza miili yao mahali hapo.
Ili
kuthibitisha kuwa lengo la muuaji kuwapeleka wahanga wake katika eneo
hilo ni ili kuwatisha na kuwajengea hofu, mmoja wa wanawake waliouawa
alikuwa amejikojolea kwenye suruali yake ya jinzi kwa hofu kabla ya
kuuawa.Wakati
Polisi wakiendelea kujitetea kutokana na mauaji ya Mtuhumiwa wa mauaji
ya kutisha David Selepe aliyeuawa Desemba 17, 1994 akiwa mikononi mwa
Polisi, walidai kwamba wana ushahidi ambao unamuhusisha David Selepe na
vifo vya wanawake sita ambao miili yao ilipatikana katika eneo la
Cleveland.
David Selepea alikuwa akituhumiwa kwa vifo vya wanawake 4, lakini alipokamatwa alikiri kuuwa wanawake 15. Ni
wakati alipokuwa akiwapeleka askari wa upelelezi katika eneo
alipotekeleza miili ya wanawake wengine ndipo alipouawa kwa kupigwa
risasi ya kichwa wakati alipojaribu kutoroka. Polisi waliamini kwamba
yeye ndiye aliyehusika na mauaji ya vifo vya wanawake hao sita.
Mwili
wa kwanza ulipatikana hapo mnamo Januari 4, 1995, ukiwa umetelekezwa
porini nusu uchi. Mwili wa mwanamke huyo haukupata kutambuliwa. Mwili
wa pili ulipatikana hapo mnamo Februari 9. Alikuwa ni mwanamke na
alikuwa uchi wa mnyama na nguo zake ziliwekwa kifuani mwake zikiwa
zimewekewa jiwe juu yake.
Alama zake za vidole ndizo zilizoharakisha
kutambuliwa kwake. Alikuwa ni binti mrembo aliyejulikana kwa jina la
Nuku Soko aliyekuwa na umri wa miaka 27. Alipotea tangu Januari pale
alipoaga kwamba anakwenda kwa dada yake aishie katika eneo la Klipgat,
na hakuonekana tangu siku hiyo.
Asubuhi
ya Machi 6, wafanyakazi wa ujenzi walikuwa wanachimba shimo katika eneo
la Atteridgevile, na walipatwa na mshtuko walipoona matiti ya mwanamke
kuashiria kwamba kulikuwa na mwili wa mwanamke uliozikwa katika eneo
hilo. Waliufukua mwili huo na baadae ulitambuliwa kwamba ni wa mwanamke
aliyetambuliwa kwa jina la Sara Matlakala Mokono.
Alikuwa na umri wa
miaka 25, na lipotea siku tatu zilizopita wakati akiwa njiani kwenda
kuonana na mtu aliyemuahidi kumpatia kazi.Mnamo
April 12 mwili mwingine uligunduliwa katika eneo la Atteridgeville.
Mwanamke huyo mikono yake imefungwa kwa nyuma kwa kutumia sidilia yake.
Alikuwa amenyongwa. Ingawa nguo zake zilikuja kuonekana katika eneo hilo
lakini chupi yake haikupata kuonekana.
Alikuja kutambuliwa baadae kama
Letta Nomthandazo Ndlangamandia aliyekuwa na umri wa miaka 25.
Mnamo
April 17, gazeti maarufu nchini humo linaloandikwa kwa lugha ya
Afikaans liliibuka na habari kwamba kuna miili ya wanawake wanne
imegunduliwa na likahitimisha kwa kusema kwamba mtindo uliotumika katika
kutekeleza mauaji hayo (modus operandi) unafanana kabisa na namna muuaji maarufu wa Cleveland alivyokuwa akiuwa ambaye anaaminika kuwa ni Davidi Selepe.
Mnamo
April 19, Polisi walitangaza rasmi kwamba kuna uwezekano kuna muuaji
mwingine anayeendesha mauaji kaika eneo hilo la Atteridgeville.
Walituhumu kwamba huenda kuna mtu anaiga mtindo wa muuaji wa Cleveland
ili kuwachanganya askari wa upelelezi.
Siku
iliyofuata mwili wa mtoto wa kiume uligunduliwa jirani kabisa na
ulipokutwa mwili wa Letta Ndlangamandla. Ilibainika kwamba mwili huo ni
wa mtoto aitwae Sibusiso aliyekuwa na umri wa miaka 2.
Mwili huo
ulikutwa umbali wa futi 65 kutoka ulipokuwa mwili wa mama yake. Letta
aliondoka mapema Mwezi April kwenda Mashariki mwa jiji la Pretoria
kukutana na mtu ambaye alimuahidi kumpatia kazi.
Kwa kuwa hakuwa na mtu
wa kumuachia mwanaye Letta aliamua kuondoka naye. Wataalamu wa uchunguzi
wa maiti walishindwa kubaini sababu ya kifo cha mtoto huyo ingawa
alikuwa na jeraha kichwani na haikujulikana ni yupi alitangulia kufa
kati ya mama au mtoto.
Kulikuwa na uwezekano kuwa mtoto Sibusiso alikufa kutokana na kupigwa na
baridi kali porini baada ya mama yake kuuawa.
Hebu fikiria mtoto mdogo
wa miaka miwili alikuwa akirandaranda porini peke yake karibu na
ulipolala mwili wa mama yake kwa sababu hakujua mahali pa kwenda
kutokana na kuwa na umri mdogo hadi alipokufa.
Mnamo
may 13, mwili wa Esther Moshibudi Mainetjas uligunduliwa katika msituni
jirani na eneo la Hercules magharibi mwa jiji la Pretoria.
Alikuwa nusu
uchi na alikuwa amenyongwa kwa kutumia nguo. Kwa mara ya mwisho
alionekana jioni ya siku iliyopita.
Mwili
wa mwanamke mwingine uligunduliwa mwezi mmoja baadae, ingawa kulikuwa
na wanawake wengine watano waliotoweka katika mazingira ya kutatanisha
kwa nyakati tofauti.
Francina Nomsa Sithebe aliyekuwa na miaka 25, mwili
wake ulikutwa ukiwa umekalishwa ukiwa umeegemea mti hapo mnamo Juni 13.
Ingawa alikuwa amevaa gauni.
wachunguzi wa maiti walibaini kwamba chupi
yake na mkanda wa mkoba wake ulikuwa umefungwa shingoni mwake na kisha
ukafungwa kwenye mti.Siku
tatu baadae, mnamo Juni 16, Elizabeth Granny Mathetsas mwili wake
uligunduliwa ukiwa uchi katika eneo la viwanda la Rosslyn kama maili 9
kaskazini magharibi mwa jiji la Pretoria. Alikuwa na umri wa miaka 19 na
mara ya mwisho alionekana akiwa hai hapo mnamo Mei 25.
Mnamo
Juni 22 mwili wa mwanamke mwingine uligunduliwa katika eneo la
Rosherville. Alikuwa amebakwa na kisha kunyongwa. Nyaraka za utambulisho
wake zilikutwa katika eneo hilo na kurahisisha kutambuliwa kwake.
alikuwa anaitwa Ernestina Mohadi Mosebo. Alikuwa na umri wa miaka 30.Siku
mbili baadae mnamo Juni 24, mwili wa Nikiwe Dikos uligunduliwa katika
eneo la Atteridgeville.
Alikuwa ametoweka tangu April 7, wakati alipoaga
kuwa anakwenda kuonana na mtu aliyemuahidi kumpatia kazi. Mwili wake
ulikuwa umeshambuliwa na mbwa mwitu kiasi cha kutawanywa vipande vpande
kila mahali. Mikono yake ilikuwa imefungwa na chupi yake.
Kutokana na
mwili wake kutawanywa na Mbwa Mwitu, Polisi walifanikiwa kupata fuvu la
kichwa chake siku iliyofuata, futi 130 kutoka yalipolala mabaki ya mwili
wake.
Alkuwa amenyongwa kwa kutumia chupi yake ikiwa imekazwa kwa
kutumia kipande cha mti, pia kulikuwa ana kipande cha mti
kilichosokomezwa kwenye uke wake. Alikuwa amevaa pete yake ya ndoa na
mabaki ya mwili huyo yalitambuliwa na mumewe.
Absolom
Sangweni alikuwa akiishi kwenye nyumba yake ya turubai katika eneo la
Beyers Park katika mji wa Boksburg. Mnamo July 17, 1995, aliwaona
mwanaume na mwanamke wakitmbea kuelekea kwenye kijipori kilichokuwa
jirani na hapo nyumbani kwake. Kwa kuwa alikuwa anajua kwamba kuna uzio
uliozungushwa katika kijipori hicho alijua watu wale wasingeweza
kuendelea na safari yao.
Aliwaita, lakini yule mwanaume alimjibu kwamba
analifahamu vizuri eneo hilo. baadae kidogo walipotea machoni mwake.
Hata hivyo Absolom aliendelea kuchunguza walipopotelea watu wale.
Baadae kidogo alimuona yule mwanaume akitokea lakini akiwa peke yake.
Absolom alidai kuona kitu kinachong’aa mkononi mwa mwanaume yule na
alikuwa akiangalia huku na huko kama vile alikuwa na wasiwasi kwamba
kuna mtu amemuona akifanya jambo na hivyo alikuwa anataka kuondoka
katika eneo hilo haraka iwezekanavyo. Hata hivyo alitoweka.
Absolom
alikwenda katika kijipori hicho na kumkuta yule mwanamke akiwa
amenyanyaswa kijinsia na alikuwa amepoteza fahamu. Absolom alikwenda
katika supermarket moja iliyokuwa jirani na kuwajulisha Polisi waliokuwa
katika eneo hilo. Sajenti
Gideon ONeal alifika katika eneo la tukio na kumkuta mwanamke huyo
akiwa amepoteza fahamu. Hakukuta mkoba wa mwanamke huyo na hivyo kupata
ugumu wa kumtambua.
Askari mwenzake aliwasili katika eneo hilo akiwa na
mkoba wa huduma ya kwanza lakini walishindwa kuokoa maisha yake.
Alifariki dunia. Alikuwa amenyongwa na mkanda wa gauni lake. Absolom
alidai kwamba alikuwa mbali na hakuweza kumtambua mwanaume huyo.Mwanamke
huyo altambuliwa kwa jina la Josephine Mantsali Mlangeni. Alikuwa na
mri wa miaka 25 na mama wa watoto wanne.
Alikuwa ameaga nyumbani kwamba
anakwenda kukutana na mtu ambaye alimwahidi kumapatia kazi nzuri.Miili mingine ya wanawake waliouawa iliogunduliwa ni hii ifuaayo:
Granny
Dimakatso Ramela. Mwili wake uligunduliwa Magharibi mwa jiji la
Pretoria. Alikuwa akiwa amelala kifudifudina kamba iliyotumika
kumnyongea ilikuwa bado iko shingoni mwake. Alikuwa na umri wa miaka 21
na alikuwa ametoweka kusikojulikana tangu Mei 23.
Mildred Ntiya Leple
aliyekuwa na umri wa miaka 28 alipelekwa Pretoria na mumewe baada ya
Granny Ramela kutoweka, ili kuonana na mtu ambaye alimwahidi kumpatia
kazi.
Hakupata kumuona mke wake tena hadi pale mwili wake ulipopatikana
hapo mnamo Julai 26 jirani na bwawa la Bon Accord karibu na mji wa
Onderstepoort, takriban maili 9 kaskazini mwa jiji la Pritoria. Alikuwa
amenyongwa kwa kutumia chupi yake.
Polisi
ilibidi waandae chumba maalum cha kufanyia uchunguzi wa miili ya
wanawake iliyokuwa ikiokotwa kila uchao baada ya kuuawa kwa mtindo
unaofanana.Mnamo
August 8, mwili mwingine wa mwanamke uligunduliwa katika mji wa
Onderstepoort.
Alitambuliwa kutokana na nyaraka zilizokutwa ndani ya
mkoba wake. Alijulikana kwa jina la Elsie Khoti Masango aliyekuwa na
umri wa miaka 25. Alikuwa ametoweka tangu Julai 14.
Mwili
wa mwanamke mwingine uligunduliwa katika eneo hilo hilo, lakini ulikuwa
umechomwa moto kiasi cha kutotambuliwa. Haikujulikana kwamba mwili ule
ulikuwa umetelekezwa katika eneo hilo kwa muda gani.
Wiki
mbili baadae mnamo Agost 23, mwili wa mwanamke mwingine aliyejulikana
kwa jina la Oscarina Vuyokazi Jakalases aliyekuwa na umri wa miaka 30
uligunduliwa jirani na eneo la Boksburg. Alikuwa ametoweka siku
ulipopatikana mwili wa Elsie Masangos. Ilikuwa ni Agosti 8.
Mnamo
Agosti 28 na 30, miili mingine ya wanawake wawili iligunduliwa katika
bwawa la Bon Accord karibu na mji wa Onderstepoort.
Mwili wa mwanamke wa
pili ulionyesha kwamba ulitelekezwa kwa miezi kadhaa katika eneo hilo,
na haukuweza kutambuliwa.Kwa
kifupi ni kwamba kwa nyakati tofauti miili zaidi ya wanawake 38
ilipatikana katika maeneo tofauti tofauti wote wakiwa wameuawa kwa
mtindo unaofanana huku wengine wakiwa wamebakwa.
Kutokana
na mauaji hayo ya kutisha na ya mfuatano, yaliwapa askari wa upelelezi
nchini humo wakati mgumu, hivyo waliamua kuwatafuta wataalamu waliobobea
kwa kazi ya upelelezi nje a nchi hiyo hususan Ulaya au Marekani.
Mmoja
wa wapelelezi wa kesi hiyo mwanamama Micki Pistorius alikwenda
kuhudhuria kongamano moja nchini Skotland mnamo Juni, ambapo alikutana
na Robert Ressler na Roy Hazelwood wote waliwahi kufanya kazi katika
shirika la upelelezi la Marekani FBI, lakini walikuwa wamestaafu wakati
huo.
baada ya kuzungumza nao walikubali kwenda nchini humo kusaidia
katika upelelezi wa kesi hiyo.Micki
Pistorius akishirikiana na Robert Rissler walitengeneza taarifa fupi
kuhusiana na mauaji huyo ili kurahisisha upelelezi wa kesi hiyo.
Taarifa
hiyo ilionyesha kwamba kulikuwa na maeneo maalum ambapo miili ya
wanawake hao iliteekezwa. Wanawake nane waliouawa walitupwa jirani na
mji wa Atteridgeville akiwepo mtoto wa kiume wa miaka miwili.
Miili ya
wanawake sita iligunduliwa katika eneo la Onderstepoort, miili ya
wanawake wengine 12 ilikutwa imetupwa katika eneo la Boksburg, pia
kulikuwa na mwanamke aliyeokotwa jirani na mji wa Cleveland. Wataalamu
hao walibaini kwamba mauaji ya wanawake 27 yalikuwa yanafanana.
Lakini pia waliamini kwamba huenda mauaji hayo yalitekelezwa na muuaji
zaidi ya mmoja. Ilionyesha kwamba maeneo ilipotelekezwa miili hiyo
ilikuwa imechaguliwa kwa umakini wa hali ya juu mno, na muuaji (wauaji)
alikuwa anawafahamu wahanga hao.
Maeneo ilipotupwa miili hiyo ilikuwa
inafikika kiurahisi na hata namna miili hiyo ilivyokuwa ikitelekezwa
muuaji hakuonekana kama alikuwaana dhamira ya kuificha ili isipatikane.
Miili mingine ilikuwa imelaliana.Katika
taarifa yao wataalamu hao pia walibainisha kwamba, wanawake wote
waliouawa kwa mujibu wa ndugu zao walikuwa wanaaga kwamba wanakwenda
kuonana na mtu aliyewaahidi kuwapatia kazi. Alikuwa anawabaka na kuwauwa
na kisha kutelekeza miili hiyo.
Walimuelezea
muuaji huyo kama ni (1)mwanaume mweusi mwenye umri kati ya mika 20 au
alikuwa anakaribia miaka 30 (2)Alikuwa amejiajiri ambapo likuwa ana
uwezo wa kuwa na fedha za kutosha. (3) huenda alikuwa anaendesha gari la
kifahari. (4)anavaa mavazi ya gharama na vito vya thamani. (5) ni mtu
anayejichanganya na watu, mcheshi na ni mtu wa wanawake. (6) kuna
uwezekani ameoa, au ametengana na mke wake au ameachana na mke wake.
(7)
ni mtu wa kujirusha kwenye vilabu na kujichanganya na watu. (8) anaweza
kuwa anajihusisha na utapeli au wizi (9) atakuwa anawafuatilia ripoti
za Polisi jinsi wanavyofanya pelelezi wao kupitia vyombo vya habari.
(10) anaonekana kuwa na chuki na wanawake ingawa anaonekana
kuwachangamkia.
(11) huwa anapiga punyeto baada ya kufanya mauaji juu ya
miili ya wanawake hao kabla ya kuitelekeza (12) anaonekana kupenda sana
wanawake na huwa anaangalia picha za ngono (13) kunauwezekano aliwahi
kunyanyaswa kijinsia alipokuwa jela hususan jela ya watoto.
(14)
anaonekana kuwa na akili sana na ni kijana wa mtaani aliyebobea kwenye
vitendo vya kihalifu.Mkoba
wa mmoja wa wanawake waliouawa na kutelekezwa katika eneo la Boksburg
ulikutwa na nyaraka ambazo ndizo zilizosababisha mwili huo utambuliwe
kuwa ni wa Amelia Rapodile. Askari wa upelelezi walipofuatilia mahali
alipokuwa akifanya kazi, wafanya kazi wenzie walidai kwamba alikuwa na
miadi na mtu aliyemtaja kwa jina la Moses Sethole mnamo Septemba 7. Hiyo
ndiyo siku aliyotoweka.
Polisi pia walikuta barua ya maombi ya kazi
kwenye taasisi ya Sethole iliyotajwa kwa jina la Youth Against Human abuse organization, ambapo alikuwa amemwahidi kumuajiri Amelia.Walipofuatilia
kwa kutumia namba za simu zilizokutwa kwenye maombi ya kazi walikutana
na mwanamke alijitambulisha kwa jina la Kwazi Sithole anayeishi katika
eneo la Wattville kusini mwa mji wa Boksburg. Alikuwa ni dada yake
Moses.
Lakini aliwambia askari wa upelelezi kwamba Sithole haishi pale
na hajulikani mahali alipo.Kuanzia
hapo askari wa upelelezi wakajua kwamba wanaye mtu sahihi aliyehusika
na mauaji hayo na si mwingine bali ni Moses Sithole.Kutokana
na taarifa za mauiaji hayo kusambaa nchi nzima, na kuleta hofu miongoni
mwa jamii ya wa Afrika Kusini, Polisi walitangaza zawadi nono kwa mtu
yeyote atakayetoa taarifa zitakazopelekea muuaji huyo kukamatwa.
Pia
aliyekuwa raisi wa chi hiyo wakati huo Nelson Mandela aliingilia kati
jambo hilo na kuwahimiza Polisi wakakikishe muuaji anakamatwa haraka
iwezekanvyo na kurejesha utulivu kwa wananchi wa nchi hiyo ambao
walikuwa wametaharuki kutokana na mauaji hayo.
Mnamo Octoba 3, mtu mmoja alipiga simu katika gazeti maarufu la The Star
la nchini humo na kuongea na mwandishi wa habari aitwae Tamsen de Beer.
Mtu huyo alijitambulisha kwa jina la Joseph Mangwena na alidai kwamba
ndiye anayehusika na mauaji Gauteng (Gauteng ni jimbo yalipo majiji la
Johannesburg na Pretoria). Kwa kauli yake mwenyewe mtu huyo alisema kwa
utulivu. “Mimi ndiye mtu ninayetafutwa kwa udi na uvumba.”
Alisema kwamba anataka kujisalimisha. Mwandishi huyo wa habari
aliwasiliana na Polisi.
Mtu huyo alipiga simu mara kadhaa katika ofisi
za gazeti hilo na simu yake ilirekodiwa. Na katika maelezo yake kwa
mwandishi huyo wa habari alieleza kwa undani jinsi alivyotekeleza mauaji
hayo. Alidai kwamba alianza kuuwa baada ya mwanamke mmoja kumtuhumu
kimakosa kwamba alimbaka ambapo alishitakiwa na kuhukumiwa kwenda jela.
Wakati alipokuwa jela aliteswa sana na wafungwa wenzake. “Nilipotoka
niliamua kulipiza kisasi.
Nilikuwa namlazimisha mwanamke ninayetaka
kumuuwa kwenda mahali ninapotaka na tunapofika hapo ninamwambia, ‘Unajua kwa nini?’
Niliteseka sana na sasa ni wakati wangu kulipiza kisasi, na ndipo
huwauwa.”
Alisema mtu huyo katika mazungmzo yake kwa njia ya simu na
mwandishi huyo wa habari. Alisema
kwamba alikuwa anatumia nguo za wahanga wake kuwanyongea na alikuwa
anapendelea chupi zao kwa sababu haziachi alama za vidole. Aliendelea
kusema kwamba baadhi ya wanawake aliowauwa walikuwa wakishuhudia maiti
za wenzao aliowaua na kutelekeza miili yao mahali hapo.
Hata
hivyo alikanusha kuhusika na mauaji ya Letta Ndlangamandla na mwanaye
wa kiume aliyekuwa na umri wa miaka 2. Alidai kwamba yeye anawapenda
watoto hivyo asingeweza kumuua mwanamke huyo wala mtoto wake.Alielezea
mahali alipotelekeza miili mingine ambayo Polisi walikuwa hawajaiona.
Kutokana na maelezo hayo waliamini kwamba huyo ndiye muuaji waliyekuwa
wakimtafuta.
Hata
hivyo kutokana na ugumu wa kumpata huyo muuaji aliyepiga simu, askari
wa upelelezi waliamua kuendelea kumtafuta mtuhumiwa wanayemfahamu Moses
Sethole. Walitoa picha zake kwenye magazeti hapo mnamo Octoba 13, na
waliwaomba wananchi wasaidie kupatikana kwa mtu huyo.
Siku
chache baada ya picha yake kuwekwa magazetini, Sithole aliwasiliana na
shemejie aliyemuoa dada yake akimuomba amtafutie bunduki ya kujilinda.
Walikubaliana na shemejie wakutane kwenye eneo la viwanda la Mintex
lililopo katika mji wa Benon ambapo atapewa hiyo silaha. Dada yake
aliwasiliana na Polisi na kuwaeleza kuhusu ombi la Sithole kwa shemejie
la kutaka atafutiwe silaha ya kujilinda. Kapteni
Vinol Viljoen na Frans van Niekerk waliona huo ndio wakati muafaka wa
kumtia muuaji huyo mbaroni.
Walikutana na uongozi wa kiwanda na
kukubaliana kuwa Inspekta Francis Mulovhedzi ajifanye ni mlinzi wa
kiwanda akae getini. Ilipofika saa 9 usiku mnamo Octoba 18, 1995,
Sithole aliwasili na kumuulizia Maxwell. Askari aliyekuwepo getini
alimwambia Inspekta Mulovhedzi aende kumtafuta Maxwell ndani ya kiwanda.
Kwa kuwa alikuwa ni mgeni pale na hakutaka kumuachia Sithole aondoke,
alikataa kwenda ndani kumtafuta Maxwell, jambo hilo lilileta ubishani
kidogo na hivyo kumfanya Sithole ajenge wasiwasi na kukimbia kutoka
katika eneo hilo.Inspekta Mulovhedzi alimfuata kule gizani
alipokimbilia. Alijitambulisha kama Afisa wa Polisi akimpigia Sithole
kelele asimame na kupiga risasi mbili hewani.
Pamoja na kwamba katika mazungumzo yake kwa njia ya simu na mwandishi wa
habari alidai kwamba anataka kujisalimisha, lakini hakujisalimisha
kirahisi kama ilivyotarajiwa. Alimjia yule Polisi akiwa na shoka. Ili
kujihami askari huyo alimpiga risasi ya miguuni hata hivyo pamoja na
kupigwa risasi lakini aliendelea kutaka kumpiga askari huyo na shoka
ambapo alimpiga tena risasi ya miguuni mpaka akaanguka.
Alikuwa amepigwa
risasi ya miguuni na tumboni hivyo alikimbizwa katika hospitali ya
Glynwood iliyoko Benoni ambapo alifanyiwa upasuaji siku iliyofuata.
Wakati
Brigedia Suike Britz Kamanda wa kitengo cha mauaji na ujambazi wa
kutumia silaha alipopata taarifa za Sithole kupigwa risasi, moyo wake
ulisimama kwa sekunde kadhaa kwa mshtuko. Baadaye akizungumzia tukio
hilo alisema,
“Ilikuwa kama déjà vu kutokana na kufanana kwa
usahihi kabisa na tukio la kuuawa kwa David Selepe, tukio ambalo hadi
sasa vyombo vya habari vimelishupalia wakitushutumu kwa uzembe. Nilisali
wakati wote nikihofu kwamba Sithole naye angekufa na nilikuwa napiga
simu kila saa ili kufuatilia hali ya afya yake.” (Déjà vu ni kitendo cha kufanana kwa jambo au matukio).
Hata
hivyo Sithole alipata nafuu na hivyo kuhamishiwa katika hospitali ya
kijeshi iliyoko katika jiji la Pritoria, ambapo ulinzi uliimarishwa.
Habari ya kukamatwa kwa Moses Sithole zilisambaa nchini humo kama moto wa mwituni.Mnamo
Octoba 28 magazeti nchini humo yaliripoti kwamba Sithole alikutwa na
Maradhi ya Ukimwi (HIV), hata hivyo Polisi hawakutoa maoni yao kuhusiana
na taarifa hizo. Ilidaiwa kwamba kuna uwezekano maradhi hayo aliyapata
kutoka kwa mmoaj wa wahanga wake aliowabaka na kuwauwa.
Wakati
huo huo askari wa upelelezi Viljoen na Frans Van Niekerk walimtembelea
Sithole hospitalini kwa ajili ya kumuhoji, lakini alikuwa mkaidi kujibu
maswali yao. Alipoingia askari mwanamke kumuhoji alikiri baadhi ya
mauaji aliyoyafanya na kitendo cha kupiga punyeto kwenye miili ya
wanawake hao baada ya kuwauwa. Mahojiano hayo yalirekodiwa.Kwa maneno yake mwenyewe Sithole alisema.
“katika
eneo la Atterdgeville niliuwa wanawake labda kumi hivi, siwezi
kukumbuka kwa usahihi, nilikuwa nawakamata kwa mikono yangu shingoni na
kuwanyonga na wakati mwingine nilikuwa natafuta kitu kama kamba ya
kuwanyongea. Nilikuwa natumia soksi ya viatu na kuwafunga shingoni na
kisha kuwanyonga. Mimi sipendi kuona damu. Nilikuwa nawalazimisha kulala
kifudifudi wakati nikiwabaka na baada ya kufanya hivyo nawanyonga na
wakati nikiwaangalia wakifa, napiga punyeto juu ya miili yao.
”Sithole
alikanusha kushirikiana na mtu yeyote katika kutekeleza mauaji hayo
lakini alisema kwamba kuna uwezekano kuna mtu mwingine aliyekuwa
akifanya mauaji sambamba na yeye. Mnamo
Novemba 3, Sithole aliruhusiwa kutoka hospitalini na kupelekwa katika
jela ya Boskburg, jela ambayo aliwahi kufungwa wakati fulani kwa kosa la
kubaka.
Jela hiyo iko jirani kabisa na eneo alilokuwa akiitelekeza
miili ya wanawake aliokuwa akiwauwa.Baadae
aliwapeleka Polisi sehemu mbalimbali ambazo alitelekeza miili ya
wanawake wengine aliowauwa ambapo baadhi ya sehemu hizo hazikupata
kujulikana na polisi.
Mnamo
Mei 20, Sithole alifikishwa mahakamani kwa mara ya kwanza na baada ya
kusomewa mashitaka kesi iliahirishwa mpaka baaba ya miezi mitano ndipo
itakapoanza kusikilizwa rasmi. Alikuwa akitetewana wakili wa kujitegemea
aitwae Eben Jordaan ambapo gharama za kumtetea zilibebwa na serikali ya
Afrika ya Kusini.
Mnamo
Octoba 28, Moses Sithole alifikiswa mahakamni na kusomewa mashikiwa kwa
makosa mauaji ya wanawake 38 akiwemo mtoto mmoja wa miaka 2, makosa 40
ya ubakaji na makosa 6 ya uporaji wa kutumia silaha. Sithole alikanusha
mashitaka hayo.
Mnamo
Desemba 5, 1997, Sithole alihukumiwa cha miaka 50 kwa kila kosa la
mauaji ya wanawake 38, miaka mingine 12 kwa kila kosa la ubakaji wa
wanawake 40 na miaka 5 kwa kila kosa la ujambazii wa kutumia silaha. Kwa
kuwa kifungo cha makosa hayo kitaenda pamoja, alitakiwa atumikie
kifungo cha miaka 2,410. Mheshimiwa
Jaji David Carstairs aliagiza atumikie angalau kifungo cha miaka 930,
ndipo afikiriwe kupewa fursa ya kutumikia kifungo cha nje (Parole).
Habari Zingine
Mjulishe Mwenzako
0 MAOINI :