ATLETICO MINEIRO MABINGWA WAPYA WA COPA LIBERTADORES!

Posted in
No comments
Thursday, July 25, 2013 By danielmjema.blogspot.com



WAKIWA kwao, Estádio Governador Magalhães, huko Belo Horizonte, Brazil, Atletico Mineiro, walipindua kpigo cha 2-0 toka Mechi ya kwanza na Alfajiri hii ya Leo kuifunga Olimpia Bao 2-0 na kutwaa Ubingwa wa Copa Libertadores, Klabu Bingwa ya Marekani ya Kusini, kwa Mikwaju ya Penati 4-3 baada Mechi kwenda Dakika 120 na Matokeo kubaki 2-0 na hivyo Jumla ya Magoli kuwa 2-2.

Hadi Mapumziko Mechi hii ilikuwa 0-0 huku Olimpia wakiutumia vyema Mfumo wao wa Kidifensi, 5-3-2, kwa kujihami sana na kuiacha Atletico wakitawala.

MAGOLI: Atletico Mineiro 2 -Dakika ya 46 Jô -87 Leonardo Silva

Lakini Kipindi cha Pili Atletico Mineiro walicharuka na kufunga Bao zao 2 na kuifanya Mechi iwe Sare kwa Jumla ya Magoli 2-2 kwa Mechi mbili na hivyo kwenda Dakika za Nyongeza 30 ambazo hazikutoa Mshindi.
Olimpia walicheza Mtu 10 kuanzia Dakika ya 85 baada ya Manzur kupokea Kadi ya Njano ya pili na hivyo kutolewa kwa Kadi Nyekundu.

Baada Dakika 120 ikaja Tombola ya Mikwaju ya Penati na Atletico Mineiro ikaibuka kidedea kwa Penati 4-3 baada ya wao kufunga Penati zao zote 4 na Olimpia kukosa mbili zilizopigwa na Miranda na Gimenez.

PENATI:

Atletico Mineiro 4-Alecsandro-Guilherme-Jô-Leonardo Silva
Olimpia 3
-Miranda [ALIKOSA]-Ferreyra-Candia-Aranda-Gimenez [ALIKOSA]

VIKOSI:

ATLETICO MINEIRO [Mfumo 4-2-3-1]: Victor, Michel, Réver, Leo Silva, Júnior César, Pierre, Josue, Tardelli, Ronaldinho, Bernard, Jo

Akiba: Rosinei, Guilherme, Alecsandro, Gilberto Silva, Leandro Donizete, Lee, Luan

OLIMPIA [Mfumo 5-3-2]: Silva, Mazacotte, Manzur, Miranda, Candia, Benitez, Pittoni, Aranda, Silva, Salgueiro, Bareiro

Akiba: Gimenez, Baez, Ferreyra, Meza, Paredes, Hermosilla, Castorino

Habari Zingine

0 MAOINI :

Fadhili Athumani



EastAfrica Swahili Blogger, Journalist at Mwanaspoti Kenya, Nairobi Kenya, Call: +254705246475, whatsapp:+255654724337, Email: fadhiliathumani85@gmail.com

Proudly Powered by EAMG .