Bartoli Bingwa Mpya Wimbledon!
Posted in
No comments
Sunday, July 7, 2013
By
danielmjema.blogspot.com
Bingwa wa mchezo wa tennis kwa wanawake katika mashindano ya Wimbledon
Marion Bartoli amesisitiza kuwa namna alivyocheza siku ya
Jumamosi(06.07.2013) huenda ni mwanzo wa ukurasa wa mafanikio yake
katika mchezo huo.
Bartoli mwenye umri wa miaka 28, ambaye alishindwa na Venus Williams katika fainali iliyopita ya Grand Slam ya Wimbledon mwaka 2007 , ni mwanamke wa tano mwenye umri mkubwa kiasi kuwa mshindi kwa mara ya kwanza wa mashindano makubwa.
Aendelea kutabasamu
Kwa upande wake Sabine Lisicki kama kawaida yake alikuwa akitabasamu huku akikiri kuwa alikuwa na wasi wasi mwingi kabla na wakati wa mchezo na kupoteza mchezo huo muhimu kwake na kwa Ujerumani kwa jumla.
Mjerumani huyo alionekana wazi kuwa fainali yake ya kwanza ya Wimbledon ilikuwa ngumu na alionekana dhahiri kuwa alikuwa anaelekea kupata kipigo cha kudhalilisha cha huenda 6-1 na 6-1. Lakini aliweza kupata ushindi katika michezo mitano mfululizo na kurejesha hali ya heshima .
Lisicki alimshinda bingwa mtetezi Serena Williams na makamu bingwa wa mwaka jana Agnieszka Radwanska katika njia yake kuelekea katika fainali, na alipigiwa upatu kumshinda Bartoli aliyeko katika nafasi ya 15 ya orodha ya wachezaji bora duniani.
Habari Zingine
Mjulishe Mwenzako
0 MAOINI :