El Baradei kuwa waziri mkuu wa Muda, Misri
Posted in
No comments
Sunday, July 7, 2013
By
danielmjema.blogspot.com
Kiongozi mkuu mwenye siasa za
wastani Mohammed El Baradei anatarajiwa kutangazwa kama waziri mkuu wa mpito
nchini Misri.
El Baradei ni mkuu wa zamani wa shirika
la masuala ya Nyuklia la Umoja wa Mataifa na pia mwanaharakati wa Upinzani.
Kwa mujibu wa shirika
la habari la taifa Al Mena, Baradei hapo jana alikutana na rais wa
muda Adly Mansoor.
Hata hivyo hatua ya Mohammed Baradei
kupewa cheo cha waziri mkuu imezua maandamano makubwa kutoka kwa wafuasi wa rais
aliyepinduliwa madarakani Mohammed Mursi.
Huku hayo yakiarifiwa hapo jana rais wa
Marekani Barack Obama amesema nchi yake haiungi mkono chama chochote cha
kisiasa nchini Misri wala kundi lolote. Obama amelaani ghasia zinazoendelea
katika maeneo tofauti nchini humo.
Siku ya Ijumaa wafuasi wa Mursi pamoja
na wapinzani wake walikabiliana vikali na kusababisha vifo vya watu 35
huku zaidi ya 1000 wakiwa wamejeruhiwa.
Habari Zingine
Mjulishe Mwenzako
0 MAOINI :