MOURINHO KUWAKOSA AZPILICUETA, MATA, TORRES MWANZO WA LIGI!
Posted in
No comments
Tuesday, July 23, 2013
By
danielmjema.blogspot.com
MSIMU
mpya wa Ligi Kuu England utaanza Agosti 17 na tayari Meneja wa Chelsea,
Jose Mourinho, ashapiga hesabu zake na kugundua katika Mechi ya
ufunguzi ya Ligi ya Timu yake dhidi ya Hull City upo uwezekano mdogo kwa
Wachezaji wake wanaocheza Timu ya Taifa ya Spain kucheza Mechi hiyo
iliyopangwa Agosti 18.
Vile vile, Mourinho sasa anatafakari Wachezaji gani awatoe kwa Mkopo kwa ajili ya Msimu mpya.
Tatizo kwa Mourinho ni kuwa kabla Ligi
kuanza zipo Mechi za Kimataifa za Kalenda ya FIFA na Chelsea inawajibika
kuwaachia Wachezaji wake kwenda huko na miongoni mwao wapo Wachezaji
watatu wa Spain, Juan Mata, Fernando Torres na César Azpilicueta, ambao
watarudi tena kujiunga na Chelsea yakiwa yamebaki chini ya Masaa 24 tu
kabla Chelsea haijacheza na Hull City Uwanja wa Stamford Bridge.
Agosti 14 Spain watacheza huko Mjini
Guayaquil Nchini Ecuador na Timu ya Taifa ya Nchi hiyo na Siku hiyo hiyo
Uwanjani Wembley, England itacheza na Scotland.
Mourinho amesema: “”Kikosi changu cha
Mechi ya Hull kitategemea Wachezaji hao hao watakaocheza Mechi za
Kimataifa Siku mbili kabla! Ikiwa Mtu anaenda Ecuador na kurudi London
Jumamosi baada ya Masaa 15 angani sidhani ataweza kucheza Jumapili!””
Tatizo hili za Mechi hizi za Kimataifa
kuchezwa Siku mbili tu kabla Ligi kuanza limelalamikiwa sana na Mameneja
wengi wa Ligi Kuu.Wakati huo huo, Mourinho ametoboa kuwa sasa anatafakari Wachezaji gani Chipukizi awatoe kwa Mkopo kwa ajili ya Msimu ujao.
Jumanne Chelsea wanatua Jakarta,
Indonesia ambako Alhamisi watacheza na Indonesia All Stars XI na Mechi
hizi ni muhimu kwa Mourinho kuwapima Chipukizi wake.Mmoja ambae atazikosa Mechi hizi ni
Kevin De Bruyne ambae aliumia huko Malaysia na kurudishwa London lakini
wengine kama Romelu Lukaku wapo Kikosini.
Tayari Mourinho ameshaamua kuwatoa kwa Mkopo Nathaniel Chalobah, Lucas Piazón na Josh McEachran ili wapate uzoefu.Chipukizi ambae ataingizwa Kikosi cha
Kwanza ni Sentahafu toka Czech, Tomas Kalas, Miaka 20, ambae alinunuliwa
kutoka Sigma Olomouc Mwaka 2010 na kukaa kwa Mkopo huko Vitesse Arnhem
kwa Miaka miwili.
Mwingine ni dogo wa Burkina Faso,
Bertrand Traore, Miaka 17, ambae Mourinho amethibitisha kuwa atapewa
Mkataba wa Mchezaji wa Kulipwa akifikisha Miaka 18.
CHELSEA-ZIARA:
May 24 Manchester City (Busch Stadium, St Louis)=KIPIGO 3-4
May 25 Manchester City (Yankee Stadium, New York)=KIPIGO 3-5
Julai 17 Singha All-Stars (Rajamangala Stadium, Bangkok)=USHINDI 1-0
Julai 21 Malaysia XI (Kuala Lumpur - BNI Cup 2013) =USHINDI 4-1
Julai 25 BNI Indonesia All-Stars (Gelora Bung Karno National Stadium, Jakarta) SAA 10 JIONI
Agosti 2 Inter Milan (Lucas Oil Stadium, Indianapolis - Guinness International Champions Cup) SAA 9 USIKU
Habari Zingine
Mjulishe Mwenzako
0 MAOINI :