GERARDO MARTINO KUMRITHI VILANOVA BARCA
Posted in
No comments
Tuesday, July 23, 2013
By
danielmjema.blogspot.com
RAIA wa Argentina, Gerardo Martino,
Kocha wa Newell’s Old Boys ya huko Argentina, anatarajiwa kutangazwa
kuwa Meneja mpya wa FC Barcelona kuchukua nafasi ya Tito Vilanova
alieondoka kwa sababu za kiafya.
Martino, mwenye Miaka 50, anategemewa kusaini Mkataba wa Miaka mitatu na kutangazwa rasmi baadae Wiki hii.
WASIFU WAKE:
JINA: Gerardo Daniel Martino
KUZALIWA: Novemba 20, 1962 (Miaka 50), Rosario, Argentina
TIMU ya VIJANA: Newell's Old Boys
KLABU:
1980–1990 Newell's Old Boys Mechi 392 Magoli: 35
1991 Tenerife Mechi 15 Goli: 1
1991–1994 Newell's Old Boys Mechi: 81 Goli: 2
1994–1995 Lanús Mechi 30 Goli 3
1995 Newell's Old Boys Mechi 15
1996 Barcelona SC Mechi 5
ARGENTINA: Mechi 1
UMENEJA:
1998 Brown de Arrecifes
1999 Platense
2000 Instituto
2002–2003 Libertad
2003–2004 Cerro Porteño
2005 Colón
2005–2006 Libertad
2006–2011 Paraguay
2012–2013 Newell's Old Boys
2013- Barcelona FC
Akiwa Nou Camp, Gerardo Martino atakuwa
pamoja na Wasaidizi wake mwenyewe ambao ni Elvio Paolorrosso, Kocha wa
Viungo, na Msaidizi Jorge Pautasso.Awali ilitegemewa Kiungo wa zamani wa
Barca, Luis Enrique, ndie atatwaa madaraka Nou Camp lakini tatizo kubwa
ni kuwa Enrique alijiunga na Klabu ya La Liga Celta Vigo Mwezi uliopita
tu na ukaja utata wa Mkataba.
Martino, au ‘Tata’ kama alivyo maarufu,
anakuwa Muargentina wa nne kuwa Kocha wa Barcelona wengine ni Helenio
Herrera, Roque Olsen na Cesar Luis Menotti na anatua Nuo Camp kuungana
na Supastaa wa Argentina Lionel Messi ambae amemsifia sana Kocha huyu.
Jumatano, Barcelona inacheza Mechi ya
Kirafiki na Mabingwa wa Ulaya, Bayern Munich na itakuwa chini Jordi
Roura kwenye Mechi hiyo iatakayochezwa huko Allianz Arena, Munich.
Habari Zingine
Mjulishe Mwenzako
0 MAOINI :