RAIS KIKWETE AMTEUA BALOZI LUMBANGA KUWA MWENYEKITI WA BODI YA PPRA
Posted in
No comments
Tuesday, July 23, 2013
By
danielmjema.blogspot.com
NA JENNIFER CHAMILA- MAELEZO

Kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa leo kwa vyombo
vya habari na Kaimu Mtendaji Mkuu wa Mamlaka ya PPRA
Laurent Shirima imeeleza kwamba uteuzi huo , umeanza rasmi
kuanzia Juni 20 ,mwaka huu ambapo Balozi Lumbanga amechukua nafasi
ya Dk.
Enos Bukuku aliyemaliza muda wake katika uongozi huo.Taarifa hiyo ilifafanua kuwa Balozi Lumbanga ni
mchumi kitaaluma,ana Shahada ya kwanza ya Uchumi ambayo ameipata katika Chuo
Kikuu cha Dares salaam(UDSM).
Pia ana Shahada ya Uzamili pamoja na Shahada ya
Uzamivu katika masuala ya Mahusiano ya Kimataifa taaluma aliyoipata chuo
cha Geneva School of Dipmacy and International Relations, Switzerland.

Amestaafu utumishi wa umma Julai mwaka jana (2012).
Balozi Lumbanga amekuwa
Mwenyekiti wa tatu wa bodi ya PPRA tangu ilipoanzishwa mwaka 2005 ambapo
Mwenyekiti wa kwanza alikuwa Bw.Philemon Luhajo na kufuatiwa na Dk.Bukuku.
KWA MSAADA WA: Father Kidevu
Habari Zingine
Mjulishe Mwenzako
0 MAOINI :