POULSEN ASISITIZA KASEJA BADO NI TANZANIA ONE
Posted in
No comments
Wednesday, July 3, 2013
By
danielmjema.blogspot.com
Siku kadhaa baada ya klabu yake ya Simba kutangaza
kumtema mchezaji wa mkongwe Juma Kaseja, kocha wa timu wa timu ya taifa ya
Tanzania Mdenmark Kim Poulsen ametangaza kikosi cha timu ya taifa na kumjumisha
Kaseja ndani ya kikosi hicho.
Poulsen
akiongea na waandishi wa habari wakati akitangaza kikosi hicho kinachojiandaa
na michuano ya CHAN na kiporo cha mechi ya kufuzu kombe la dunia dhidi ya
Gambia, alisema amekuwa akisoma na kusoma sana habari zinamhusu Kaseja na klabu
yake kupitia kwenye vyombo vya habari, lakini yeye kwa upande wake amesema bado
anamuamini Kaseja na ataendelea kuwa mchezaji muhimu ndani ya kikosi chake:
"Nimekuwa nikisikia
taarifa nyingi zinamhusu nahodha wetu Juma Kaseja, ningependa kuweka suala hili
wazi kwamba Kaseja bado ni mchezaji mzuri na anafanya kazi nzuri sana ndani ya
timu ya taifa.
Ni nahodha mzuri kwa sababu ni kiongozi mzuri kwa wenzie nje na
ndani ya uwanja. Hivyo kwangu hali itaendelea kuwa vile vile na nategemea kesho
kumuona akijiunga na kambi ya timu ya taifa, ataendelea kuwa nahodha na pia
golikipa namba 1 wa kikosi changu.
Kuhusu yeye na klabu yake nisingependa
kuyaingilia, lakini kwangu Kaseja bado ni muhimu kwa sababu amekuwa akifanya
nzuri kwenye timu ya taifa. Kuhusu hatma ya huko mbele, tusubiri muda
utaongea," alisema Kim Poulsen.
Wachezaji wengine walioitwa kwenye timu ya Taifa ni kama ifuatavyo:
Wachezaji wengine walioitwa kwenye timu ya Taifa ni kama ifuatavyo:
Makipa
Juma Kaseja
Ally Mustapha
Mwadini Ally
Aishi Mwanula.
Mabeki
Aggrey Morris
Kevin Yondani
Canavaro
Shoamari Kapombe
Erasto
Vicent
David
Luhende
Viungo
Mcha Khamis
Kazimoto
Sure Boy
Domayo
Chanongo
Kiemba
Washambuliaji
Mrisho Ngassa
Simon
Msuva
John Bocco
Juma
Habari Zingine
Mjulishe Mwenzako
0 MAOINI :