RC-GAMA AKABIDHI GARI KWA HALMASHAURI YA SAME
Posted in
No comments
Wednesday, July 10, 2013
By
danielmjema.blogspot.com
RC-Gama akifungua mlango wa Gari kuashiria uzinduzi, Kulia ni Mkuu wa Wilaya ya Same Herman Kapufi. |
katika makabidhiano hayo Gama amemtaka Mwenyekiti wa wilaya ya Same, Christopher Ilila kuiingia mkataba wa makabidhiano wa vifaa na watendaji wake wote ili kuwabana watumishi wabadhirifu.
Mkuu huyo wa Mkoa wa Kilimanjaro pia, amewataka viongozi wa Halmashauri ya wilaya ya Same kutumia gari hilo kwa manufaa ya wananchi na sio yao binafsi.
Amesema kuwa Gari hilo limetengwa kwa ajili ya kutumika katika idara ya fedha, kitengo cha mapato pamoja na kazi nyinginezo ili kuweza kuboresha shughuli za ukusanyaji wa mapato katika halmashauri hiyo lakini sio vibaya kama gari hilo litatumika kusaidia wananchi kwani wao ndio walengwa wakuu.
Aidha Gama ameipongeza Halmashauri hiyo kwa kutafuta njia mbadala wakuongeza mapato katika Halmashauri huku akitahadharisha kuwashughulikia watumishi wabadhilifu ambao huingiza ubadhilifu
katika mradi huo. (Habari zote na Kija Elias, Same)
Habari Zingine
Mjulishe Mwenzako
0 MAOINI :