MATOKEO KIDATO CHA NNE HADHARANI
Posted in
Elimu
No comments
Friday, February 21, 2014
By
danielmjema.blogspot.com
Naibu Katibu mkuu NECTA, Dkt. Charles Msonde |
MATOKEO ya Kidato cha nne kwa 2013 yametangazwa huku
watahiniwa 235,227 wakifaulu mtihani huo ikiwa ni sawa na asilimia
58.25 ya waliofanya mtihani huo. Jumla ya wanafunzi 404,083 walifanya
mtihani huo huku waliofaulu kwa daraja la I-III wakiwa wanafunzi 74,324
sawa na asilimia 21.09 ya waliotahiniwa.
Kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa na Baraza la Mitihani la Taifa
(NECTA) leo jijini Dar es Salaam, shule 10 za sekondari zilizofanya
vizuri (zilizoongoza) ni pamoja na St. Francis Girls, Marian Boys, Feza
Girls, Precious Blood, Canossa, Marian Girls, Abbey, Anwarite Girls,
Rosmini na Don Bosco Seminary.
Akitangaza matokeo hayo mbele ya waandishi wa habari, Kaimu katibu mkuu wa NECTA, Dk. Charles Msonde, alisema katika matokeo ya mwaka 2013, shule kumi za sekondari zilizofanya
vibaya zaidi ni pamoja na Singisa Sekondari, Sekondari ya Hurui,
Sekondari ya Barabarani, Sekondari ya Nandanga, Sekondari ya Vihokoli,
Sekondari ya Chongoleani, Sekondari ya Likawage, Sekondari ya Gwandi,
Sekondari ya Rungwa na Sekondari ya Uchindile.
Taarifa hiyo ilifafanua zaidi kuwa kati ya watahiniwa 404,083 waliofanya mtihani
wasichana waliofaulu ni 106,792 huku idadi ya wavulana waliofaulu
ikifikia 128,435. Wavulana waliopata daraja la kwanza (division one) ni
5,030 huku idadi ya wasichana ikiwa ni 2,549.
Aidha wavulana waliopata daraja la tatu (division three) ni 27,904 na
wasichana ni 17,113. Wanafunzi waliopata daraja la nne (division four)
ni 126,828, huku idadi ya wasichana wakiwa 62,841 na wavulana 63,987.
Taarifa imefafanuwa kuwa jumla ya wanafunzi 151,187 wamepata sifuri
(division ziro), ambapo idadi ya wasichana ni 72,237 na wavulana ni
78,950.
Habari Zingine
Mjulishe Mwenzako
0 MAOINI :