UVCCM WAFANYA BARAZA LA WILAYA NA KUCHAGUA VIONGOZI WAPYA WA MAJIMBO, TEMEKE
No comments
Sunday, February 16, 2014
By
danielmjema.blogspot.com
Mbunge wa Kigamboni Ndugu Faustine Ndungulile (aliyevaa
kovia na ameshika kipaza sauti) akiwa tayari meza kuu. Kulia kwake ni
Mwenyekiti wa Vijana (W) Temeke Ndugu Oliver Mwambope, Katibu wa UVCCM
(W) Temeke Ndugu Amour Onesha, Katibu Uhamasishaji na Chipukizi (W)
Temeke Ndugu Sabuni. Kushoto kwa Mbunge Ndugu Ndungulile ni Wajumbe wa
Kamati ya Utekelezaji (W) Temeke Fanny Abdul, Ernest Mwingira na Fikiri
Mzome. Picha na Emmanuel Shilatu
Mgeni
rasmi ambaye pia ni Mbunge wa jimbo la Kigamboni Ndugu Faustine
Ndungulile akifungua rasmi Baraza la kazi la UVCCM (W) Temeke mbele ya
Wajumbe (hawapo pichani) lililofanyika kwenye ukumbi wa Malaika uliopo
Kata ya vijibweni, Jimbo la Kigamboni.
Wagombea wa nafasi za Uenyekiti na Ukatibu wa Majimbo ya Kigamboni na Temeke ya UVCCM.
Mmojawapo
wa wagombea ambaye alikuja kushinda nafasi ya Uenyekiti wa Jimbo la
Kigamboni kupitia UVCCM akichukua karatasi ya kupigia kura.
Mjumbe wa Baraza la UVCCM, Ndugu Emmanuel John akichukua karatasi ya kupigia kura.
Mjumbe wa Baraza Ndugu Dude akipiga kura yake.
Mjumbe wa Baraza Ndugu Yasin Kanyama akiikusanya kura yake aliyoipiga.
Mjumbe wa Baraza la Vijana UVCCM Ndugu Emmanuel John akiikusanya kura yake aliyoipiga. Picha zote na Emmanuel Shilatu
**********
Na
Emmanuel J. Shilatu
Umoja
wa Vijana wa Chama Cha Mapinduzi wilaya Temeke wamefanya Baraza la Wilaya
kikatiba lililokuwa ni Baraza la kikazi zaidi ambapo pamoja na mambo mengineyo
walifanya uchaguzi wa majimbo yaliyopo ndani ya Wilaya hiyo na kupata Wenyeviti
na Makatibu wapya wa majimbo.
Baraza
hilo la Vijana ambalo lilifunguliwa na Mgeni rasmi Mbunge wa Kigamboni, Ndugu
Faustine Ndungulile ambaye wakati wa ufunguzi aliwaasa vijana kujiepusha na
matumizi ya madawa ya kulevya na kujikinga zaidi na maambukizi ya virusi vya
ukimwi kwani hali iliyopo inatisha sana kwa vijana.
“Kati
ya vijana wa kike watatu wanaotumia madawa ya kulevya, wawili kati yao ambao ni
asilimia 67 wameathirika na virusi vya ukimwi. Halikadhalika kwa upande wa
vijana wa kiume wawili wanaotumia madawa ya kulevya, mmojawao ambaye ni
asilimia 50 ana maambukizi ya virusi vya ukimwi. Hali ni mbaya sana kwa vijana.”
Alisema Mhe. Ndungulile.
Ndugu
Ndungulile ambaye pia ni Mjumbe wa kamati ya siasa ya wilaya ya Temeke aliwaasa
na kuwatia moyo vijana kujitokeza kugombea nafasi mbalimbali za kiuongozi
katika uchaguzi wa serikali za mitaa na
uchaguzi mkuu hapo mwakani naye kwa nguvu zake zote atapambana katika kuwatetea
vijana wenye sifa stahiki kwani anaamini vijana ni nguvu kazi ya sasa ya Taifa.
Ndugu
Ndugulile aliwaasa na kuwatakia uchaguzi mwema wajumbe wa Baraza hao wachague
viongozi wenye sifa wanaowataka kwani yeye kama Ndugulile ameanika waziwazi
kuwa hajashirika hata chembe katika kupanga safu za viongozi badala yake jukumu
hilo limeangukia mikononi mwao wajumbe hao.
Kwenye
baraza hilo la Vijana ambalo lilikuwa ni baraza la kazi waliwachagua viongozi
wa majimbo ya kigamboni na Temeke yanayopatikana ndani ya Wilaya ya Temeke.
Kwa
upande wa jimbo la Temeke waliojitokeza kuomba nafasi ya Uenyekiti ni Arnord Sangawe aliyepata kura 48, Julius Mkada
aliyepata kura 24 na Peter Sillo aliyepata kura 4. Mshindi wa nafasi ya
Uenyekiti wa Jimbo la Temeke UVCCM ulinyakuliwa na Arnord Sangawe.
Halikadhalika
waliojitokeza kwenye nafasi ya Ukatibu walikuwa ni Athumani Nyamlani aliyepata
kura 6, Juma Ndwangila aliyepata kura 59 pamoja na Laurence Limwata aliyeapata
kura 11. Hivyo nafasi ya Ukatibu wa jimbo ulichukuliwa na Ndugu Juma Ndwangila.
Kwa
upande wa jimbo la Kigamboni wagombea wa nafasi ya Uenyekiti wa jimbo walikuwa ni Ally Makwilo
aliyepata kura 28, Shaaban Mbegu aliyepata kura 7 na Yasin Kanyama aliyepata
kura 43. Hivyo Yasin Kanyama akatangazwa ndiye mshindi wa Uenyekiti wa jimbo la
Kigamboni kupitia UVCCM.
Halikadhalika
upande wa makatibu wagombea wa jimbo la Kigamboni walikuwa ni Kambarage
Makongoro aliyepata kura 27, Mustaffa Pilla aliyepata kura 32 na Salum mpili
aliyepata kura 16 na matokeo hayo yalimpa ushindi Ndugu Mustafa Pilla kuwa
ndiye Katibu wa jimbo la Kigamboni kupitia UVCCM.
Habari Zingine
Mjulishe Mwenzako
0 MAOINI :