SEHEMU YA USHAHIDI KESI YA OSCAR PISTORIUS KUBANWA.
Posted in
Mahakamani ya kimataifa
No comments
Monday, March 10, 2014
By
danielmjema.blogspot.com
Mwanariadha mlemavu wa Afrika
Kusini Oscar Pistorius, ametapika mahakamani huku akisikia ushahidi
kutoka kwa mtaalamu wa uchunguzi wa mauaji katika kesi dhidi ya
Pistorius.
Upande wa mashitaka unanuia kuthibitisha kuwa bwana Pistorius alimpiga risasi maksudi aliyekuwa mpenzi wake Reeva Steenkamp mwaka jana wakati wawili hao walipokuwa wanagombana.Pistorius amekanusha madai hayo akisema kua alimpiga risasi Reeva kwa bahati mbaya akidhani alikuwa jambazi aliyekuwa amevamia nyumba yao.
Wakati huohuo jaji anayesikiliza kesi hiyo amepiga marufuku kupeperusha kesi dhidi ya Oscar moja kwa moja kutoka mahakamani wakati ambapo picha za mauaji ya Reeva zitakapoonyeshwa.Pistorius alitapika mahakamani aliposikia ushahidi kuhusu mauaji ya Reeva na kuona picha hizo.
Bwana Saayman alimshawishi jaji kutoruhusu kuonyeshwa kwa picha hizo akisema kuwa zinaonyesha majeruhi mabaya aliyoyapata Reeva na kwamba ni lazima mahakama iweze kumsitiri marehemu. Jaji huyo pia alipiga marufuku mjadala wowote kuhusu picha hizo kwenye Twitter.
Habari Zingine
Mjulishe Mwenzako
0 MAOINI :