MATUKIO MBALIMBALI KATIKA AJALI YA TRENI ILIYOCHUKULIWA NA MAFURIKO
No comments
Wednesday, April 2, 2014
                      By 
                      danielmjema.blogspot.com
Sehemu
 ya mabehewa ya mafuta na ngano ambayo hayakusombwa na maji katika ajali
 iliyotokea usiku wa kuamkia leo katika stesheni ya Gulwe, hiyo imetokea
 saa 9.15 usiku. Treni hiyo ya Mizigo ilikuwa ikitokea Dar es Salaam na 
kuelekea Mkoani Kigoma na ilikuwa na mabehewa yaliyobeba ngano, sukari 
na mafuta.
Njia
 ya Reli iliyoondolewa na maji katika stesheni ya Gulwe Wilaya ya 
Mpwampwa kutokana na mvua kubwa zinazoendelea kunyesha maeneno mbambali 
nchini.
Katibu
 Mkuu wa Wizara ya Uchukuzi, Dk. Shaaban Mwinjaka akitoka kwenye maji 
baada ya kuangalia kichwa cha treni kilichopata ajali na kusombwa na 
maji katika stesheni ya Gulwe, Wilaya ya Mpwampwa, usiku wa kuamkia leo,
 kutokana na mvua zinazoendelea kunyesha sehemu mbalimbali za nchi. 
Ajali hiyo imesababisha kifo cha watu wawili na wengine saba kujeruhiwa 
na kulazwa katika hospital ya Benjamin Mkapa iliyoko wilayani Mpwampwa.
Katibu
 Mkuu wa Wizara ya Uchukuzi, Dk, Shaaban Mwinjaka akimfariji mmoja wa 
Majeruhi wa Ajali ya treni ya mizigo iliyotokea katika Stesheni ya Gulwe
 Bw. Michael Lupatu wakati alipomtembelea katika hospitali ya Benjamin 
Mkapa iliyopo Wilayani Mpwampwa leo mchana. Ajali hiyo ya treni ya 
mizigo imetokea usiku wa kuamkia leo na kusababisha kifo cha watu wawili
 na wengine saba kujeruhiwa.
(Picha na kitengo cha Mawasiliano Serikalini uchukuzi)
Habari Zingine
Mjulishe Mwenzako

0 MAOINI :