WANAHABARI WATEMBELEA GEREZA KUU LA WANAWAKE KINGOLWIRA - MOROGORO, WAMPONGEZA KAMISHNA JENERALI MINJA KWA JUHUDI KUBWA ZA MABORESHO NDANI YA MAGEREZA NCHINI
Posted in
Jicho la Habari
No comments
Saturday, December 20, 2014
By
danielmjema.blogspot.com
Mkuu wa Gereza Kuu la Wanawake Kingolwira, Mrakibu Mwandamizi wa Magereza, Loyce Ruhembe akiwakaribisha Wanahabari ambao wakitembelea gerezani hapo Desemba 19, 2014. Wanahabari hao wapo katika ziara ya kikazi katika miradi mbalimbali ya Uzalishaji mali inayotekelezwa kwa mafanikio makubwa na Jeshi la Magereza(kushoto) ni Mkuu wa Magereza Mkoani Mororogoro, Kamishna Msaidizi Mwandamizi wa Magereza, Kato Rugainunula.
Wafungwa wa kike wa Gereza Kuu la Wanawake Kingolwira - Morogoro wakifuma mashuka katika Kiwanda cha Ushonaji cha Gereza hilo. Wafungwa hao wanapitiwa ujuzi wa aina mbalimbali ikiwemo Ushonaji wa nguo ikiwa ni sehemu ya utekelezaji wa Programu za Urekebishaji ndani ya Magereza hapa nchini.
Muonekano wa mashuka na mito yake yanayofumwa na Wafungwa Wanawake katika Kiwanda cha Ushonaji cha Gereza Kuu la Wanawake Kingolwira - Morogoro.
Wanahabari wakionja chakula cha Wafungwa katika Gereza Kuu la Wanawake Kingolwira - Morogoro walipotembelea Gereza hilo Desemba 19, 2014(kulia) ni Mwandishi kutoka Gazeti la Habari Leo, Bi. Regina Kumba(kushoto) ni Mwandishi kutoka Gazeti la Daily News, Bw. Finning Simbeye(katikati) ni Mwanahabari kutoka Mamlaka ya Vitambulisho vya Taifa, Bi. Rose Mdami.
Mkuu wa Gereza Kuu la Wanawake Kingolwira - Morogoro, Mrakibu Mwandamizi wa Magereza, Loyce Ruhembe akipokea rasmi msaada wa vitu mbalimbali vilivyotolewa na Wanahabari hao kwa ajili ya Wafungwa wa kike gerezani hapo walipotembelea Gereza hilo Desemba 19, 2014.
Mkuu wa Gereza Kuu la Wanawake Kingolwira - Morogoro, Mrakibu Mwandamizi wa Magereza, Loyce Ruhembe akikabidhi msaada huo kwa Mfungwa wa Kike ambaye ndiye Nyampara Mkuu wa Gereza Kuu la Wanawake Kingolwira - Morogoro. Wafungwa wa Gereza hilo wamewashukru Wanahabari hao kuwatembelea pamoja na msaada huo walioutoa na wameahidi kuwa raia wema mara wamalizapo vifungo vyao.
Msaada wa vitu mbalimbali vya Kibinadamu na vinavyoruhusiwa Magerezani vilivyokabidhiwa na Wanahabari walipotembelea Gereza Kuu la Wanawake Kingolwira - Morogoro Desemba 19, 2014.
Habari Zingine
- Nawaza kwa Sauti: Leo Nimemkumbuka Shujaa Patrice Lumumba
- Katibu Mkuu amuaga rasmi Balozi wa Finland aliyemaliza muda wa kazi nchini
- KATIBU MKUU WIZARA YA MAMBO YA NJE AONGOZA MAADHIMISHO YA SIKU YA TAIFA LA SWEDEN
- WIZARA YA MAMBO YA NJE NA USHIRIKIANO WA KIMATAIFA WAFANYA MKUTANO MKUBWA JIJINI DAR ES SALAAM KUJAILI MCHANGO WA DIPLOMASIA KATIKA KUFIKIA DIRA YA TAIFA 2025
- Africa Day 2015 is an opportunity to celebrate the development of the African continent as well as consider the various opportunities that it offers - DHL
Mjulishe Mwenzako
0 MAOINI :