Washindi wa shindano la AppStar wakabidhiwa zawadi zao

Posted in
No comments
Sunday, December 21, 2014 By danielmjema.blogspot.com


Mshindi wa kwanza wa shindano la AppStar tabaka la wabunifu waliobobea Roman Mbwasi akielezea jambo wakati wa shughuli ya kukabidhi zawadi kwa washindi hao iliyofanyika makao makuu ya Vodacom Tanzania mwishoni mwa wiki hii. Katikati ni Meneja Uhusiano wa Nje wa Vodacom Abigail Ambweni, akimsikiliza kwa makini pamoja na mshindi wa kwanza katika tabaka la wabunifu chipukizi, George Machibya (kulia) Shindano hilo linaendeshwa na kampuni hiyo.

Meneja Uhusiano wa Nje wa Vodacom Tanzania Abigail Ambweni (kushoto) akishuhudia wakati mshindi wa kwanza wa shindano la AppStar tabaka la wabunifu waliobobea Roman Mbwasi (wa pili kutoka kushoto) akionyesha zawadi ya pesa taslimu Tsh. milioni 2/- aliyojishindia kupitia shindano la AppStar. Wakishuhudia tukio hilo pia ni mshindi wa kwanza katika tabaka la wabunifu chipukizi, George Machibya (wa tatu toka kushoto) na Athumani Mahiza, mshindi wa pili katika tabaka la wabunifu waliobobea (wa mwisho toka kushoto). Shindano hilo linaendeshwa na kampuni hiyo.

Meneja Uhusiano wa Nje wa Vodacom Tanzania Abigail Ambweni (kushoto) akimkabidhi zawadi ya pesa taslimu Tsh. milioni 2/- mshindi wa kwanza wa shindano la AppStar tabaka la wabunifu waliobobea ambao programu zao tayari zinatumiwa na watu zaidi ya 50,000 Roman Mbwasi (wa pili toka kushoto). Shindano hilo linaendeshwa na kampuni hiyo.

Washindi wa shindano la AppStar wakionyesha zawadi zao za pesa taslimu walizokabidhiwa na Meneja Uhusiano wa Nje wa Vodacom Tanzania Abigail Ambweni (wa tatu toka kushoto) Hafla hiyo ilifanyika makao makuu ya kampuni hiyo mwishoni mwa wiki. Shindano hilo linaendeshwa na kampuni hiyo.

Meneja Uhusiano wa Nje wa Vodacom Tanzania Abigail Ambweni akiwaeleza jambo washindi wa kwanza wa shindano la AppStar wakati wa shughuli ya makabidhiano ya zawadi iliyofanyika makao makuu ya kampuni hiyo mwishoni mwa wiki. Katikati ni Roman Mbwasi mshindi wa kwanza wa shindano hilo katika tabaka la wabunifu waliobobea na kushoto ni George Machibya mshindi wa kwanza katika tabaka la wabunifu chipukizi wakisikiliza kwa makini.

Habari Zingine

0 MAOINI :

Fadhili Athumani



EastAfrica Swahili Blogger, Journalist at Mwanaspoti Kenya, Nairobi Kenya, Call: +254705246475, whatsapp:+255654724337, Email: fadhiliathumani85@gmail.com

Proudly Powered by EAMG .