NJAA INAUA WATOTO SOMALILAND

No comments
Monday, March 28, 2016 By danielmjema.blogspot.com

Baa la njaa limesababisha vifo vya watoto na mifugo kufuatia ukame wa miaka miwili Somaliland. Maafisa wa serikali iliyojitangaza huru ya Somaliland wameiambia kituo cha BBC kuwa hofu imeanza kutanda baada ya mvua kukosa kunyesha kwa mwaka wa pili mfululizo katika maeneo ya Magharibi wa jimbo hilo lililojitenga kutoka kwa jamhuri ya Somalia.


Ali Hamud Djibril amesema kuwa watoto kadhaa wameaga dunia huku maelfu ya mifugo ikifa kufuatia ukame huo uliodumu kwa misimu mwili. Eneo hilo la Magharibi lilikuwa limewapokea wakimbizi kutoka Ethiopia lakini hali imezidi kuzorota Somaliland.

Umoja wa mataifa unasema kuwa maelfu kwa mamia ya watu wanahitaji msaada wa dharura Somaliland na mashariki mwa Somalia.

Habari Zingine

0 MAOINI :

Fadhili Athumani



EastAfrica Swahili Blogger, Journalist at Mwanaspoti Kenya, Nairobi Kenya, Call: +254705246475, whatsapp:+255654724337, Email: fadhiliathumani85@gmail.com

Proudly Powered by EAMG .