Ukivuta sigara kwenye maeneo ya umma, mighahawa na maeneo ya burudani faini dola 60 nchini Uganda
Posted in
afrika mashariki
,
Afya
No comments
Thursday, May 19, 2016
By
danielmjema.blogspot.com
Sheria mpya kali dhidi ya uvutaji na mauzo ya bidhaa za tumbaku zimeanza kutekelezwa nchini Uganda. Watu wanaovuta sigara wakiwa maeneo ya burudani na migahawa sasa watapigwa faini ya dola 60 au kifungo cha hadi miezi miwili jela.
Pia wavutaji sigara watahitajika kuwa umbali wa takriban mita 50 kutoka maeneo ya umma kama vile shule na hospitali.Sheria hizo pia zinapiga marufuku kuuzwa kwa sigara za elektroniki pamoja na shisha ambavyo ni maarufu kwenye maeneo ya burudani mjini Kampala.
Serikali pia imepiga marufuku kuuzwa kwa sigara moja na kudhibiti zaidi matangazo ya sigara na kuzwa kwa bidhaa za tumbaku kwa watu walio chini ya umri wa miaka 21.
Habari Zingine
- UHURU WA HABARI SIO KUIANGALIA TU SERIKALI - MWAKYEMBE
- JUKWAA LA WAHARIRI TANZANIA LATANGAZA KUSUSIA KUANDIKA HABARI ZA MKUU WA MKOA WA DAR
- WENGI WALIVYOJITOKEZA KUMUAGA MWANA TBN JENNIFER LIVIGHA (CHINGA ONE) HOSPITALI YA AMANA JIJINI DAR
- Wachimbaji mgodi 15 waliokwama ardhini waokolewa nchini Tanzania
- Al-Shabab washambulia kambi ya majeshi ya Kenya nchini Somalia
- Fahamu nchi zinaongoza kwa matumizi ya Bangi
- Kuwa na mpenzi na afya nzuri huchangia furaha
- Mji wa Dodoma, nchini Tanzania yakumbwa na ugonjwa usiojulikana
- Tanzania kinara unyanyasaji kwa watu wenye Ualbino
- Je Wajua Samaki Wabichi ni Dawa?
Mjulishe Mwenzako
0 MAOINI :