Ureno inahitaji kuifunga Hungary ili kusonga

Posted in
No comments
Monday, June 20, 2016 By danielmjema.blogspot.com

Kama ni mpenzi wa michuano ya Euro 2016, usisahau kuwa kuna michezo mitatu imechezwa June 18 2016, moja kati ya mchezo uliochezwa usiku wa June 18 ni mchezo kati ya Ureno dhidi ya Austria, huu ulikuwa ni mchezo ambao Ureno na  Austria zote zilikuwa zinahitaji ushindi.
ro1
Cristiano Ronaldo ambaye ndio nahodha wa Ureno, alishindwa kuiongoza timu yake iibuke na ushindi dhidi ya Austria na matokeo yake wakaambulia sare ya pili mfululizo katika mchezo wao wa pili wa Kundi F, mchezo huo ulimalizika kwa sare ya 0-0,wakati nyota wa Ureno Cristiano Ronaldo tulishuhudia akikosa penati dakika ya 79.
ro 4
Msimamo wa Kund F
Kwa matokeo hayo maisha ya timu ya taifa ya Ureno kuendelea kusalia katika michuano ya Euro 2016, ni kuhakikisha wanapata ushindi katika mchezo wao wa mwisho wa Kundi F dhidi ya Hungary wanaoongoza msimamo wa Kundi hilo kwa kuwa na jumla ya point nne na Ureno wakisalia nafasi ya tatu nyuma ya Iceland.
ro
Mwisho wa mchezo huo shabiki alivamia uwanja na kukimbilia kupiga self naCristiano Ronaldo

Habari Zingine

0 MAOINI :

Fadhili Athumani



EastAfrica Swahili Blogger, Journalist at Mwanaspoti Kenya, Nairobi Kenya, Call: +254705246475, whatsapp:+255654724337, Email: fadhiliathumani85@gmail.com

Proudly Powered by EAMG .