Guzo mitandaoni: Thamani ya Barua ya Mohammad Ali kwa Mandela

Posted in
No comments
Monday, December 19, 2016 By danielmjema.blogspot.com

Barua iliyowekwa sahihi na mwanamasumbwi Mohammad Ali na kuandikiwa rais wa zamani wa Afrika Kusini Nelson Mandela, akitoa rambu ramba zake kufuatia kuawa kwa mtu aliyekuwa akipinga ubaguizi wa rangi imeuzwa kwa pauni 7,200.
Muuzaji wa barua hiyo Andrew Aldridge alisema, "ni vyema kuwa Mohammad Ali alikuwa mwanamichezo bora zaidi hukui naye Nelson Mandela akiwa mtu mashuhuri zaidi katika karne iliyopita.
Barua hiyo ilipiwa chapa cha msaidizi wa meneja wa hoteli ya Elangeni iliyo mjini Durban ambapo Ali alikuwa akiishi wakati huo. Barua hiyo iliyouzwa kwa mnunuzi kutoka nchini Marekani ilitarajiwa kuuzwa kwa kati ya dola 6,000 na 8,000.
Muhammad Ali alikuwa nchini Afrika Kisini kwa kipindi kifupi mwezi Aprili mwaka 1993 baada ya kuwasili muda mfupi baada ya kuuliwa kwa Chris Hani tarehe 10 mwezi Aprili.
Hani alikuwq kamanda wa kundi la Umkhonto We Sizwe, kundi lililojihami la ANC. Alikuwa mkosoaji mkubwa wa serikali ya ubaguzi wa rangi na aliuaw mkereketwa mmoja nje ya nyumba yake eneo la Boksburg.
BBC

Habari Zingine

0 MAOINI :

Fadhili Athumani



EastAfrica Swahili Blogger, Journalist at Mwanaspoti Kenya, Nairobi Kenya, Call: +254705246475, whatsapp:+255654724337, Email: fadhiliathumani85@gmail.com

Proudly Powered by EAMG .