SIMU YAMPONZA MWANAFUNZI WA MSASANI SEKONDARI, APEWA KIPIGO CHA MBWA MWIZI...

Posted in
No comments
Sunday, June 30, 2013 By danielmjema.blogspot.com



KIBAKA Rajabu Hamisi Juma (15), Mwanafunzi wa shule ya Sekondari ya Msasani, iliyoko Manispaa ya Moshi, Mkoani Kilimanjaro, amenusurika kuuwawa na wananchi wenye Hasira kali baada ya kufamaniwa mchana wa leo akiiba katika Duka la mfanyabiashara Paulo Maile.

Kibaka huyo ambaye ni mkazi wa Pasua, amekutwa na masahibu hayo baada ya kuingia dukani hapo kwa kudhani kuwa mhudumu wa duka yuko mbali na ndipo alipokutwa akiwa tayari ameshaiba Simu, aina ya Nokia huku akijaribu kuficha Laptop iliyokuwa dukani hapo.

Akizungumzia mkasa huo, kibaka Rajabu huyo aliamua kufanya hivyo kwa ajili ya kukosa ada ya kulipa shule kutokana na wazai wake kukataa kumlipia ada anayodaiwa shuleni hapo.



Tukio hilo lililowaacha mdomo wazi baadhi ya mashuhuda waliofika dukani hapo , limetokea leo majira ya saa 6:10 mchana katika duka la Nguo lililloko katika mtaa wa double Road, barabara kuu ya Moshi-Dar es salaam linalomilikiwa na mfanyabiashara Paulo Maile mkazi wa Soweto.


Kamera ya TAIFA LETU.com ilifika katika eneo la tukio na kukuta kijana huyo akishushiwa kipondo na mhudumu wa duka hilo aliyefahamika kwa jina moja la George.Huu hapa ni mkanda mzima wa tukio lenyewe:
Amando Tarimo ambaye ni mmoja wa mashuhuda wa tukio hilo akishusha kipondo kwa kijana Rajabu Hamisi aliyekutwa akijaribu kuiba katika duka la mfanyabiashara Paulo Maile, Leo Mchana.


Duka la maile lililoibiwa leo lafungwa muda mfupi baada ya jaribio hilo kuzimwa na wasamaria wema

Gari la Maile lilikiwa ilmeachwa nje ya duka hilo, Maile alilazimika kuongozana na Polisi kutoa maelezo ya mkanda mzima

Gari la Polisi likiondoka na mhalifu katika eneo la tukio

Vijana wa Boaz wakiondoka na Kibaka huyo aliyenusirika kufa mikononi mwa Raia Wema

George akitoa Maelezo kwa mashuhuda wa tukio la wizi nje ya duka hilo

George aendelea na Maelezo

Kibaka  Rajabu Hamisi (Jezi ya Manchester Utd) akiomba msamaha baada ya kufumaniwa dukani katika jaribio la wizi, Paulo Maile ambaye ndiye mmiliki wa Duka (shati la mistari), George (shati jekundu katikati) na mmoja wa mashuhuda wakimsikiliza kibaka huyo dukani hapo

Rajabu akipakizwa kwenye gari la polisi leo mchana

Mwenye duka akitoa kipondo kwa Kibaka huyo...

kipondo kikiendelea...

shughuli ndani ya duka...

Maile akiendeleza kichapo cha hatari...
 
Maile akizuiliwa na baadhi ya mashuhuda wa tukio hilo

Mmoja wa Mashuhuda wa tukio hilo, Amando Tarimo akiendeleza kipondo kwa kibaka huyo....

Mhudumu wa duka hilo akipiga simu Polisi...
 
Jirani wa Duka Hilo, Mzee Harambee akizuliwa na msamaria mwema....
 
Vijana wa Boaz wakiondoka na kibaka eneo la Tukio....

Kibaka Rajabu akibubujikwa na machozi baada ya kukutwa ndani ya duka hilo...

Hapa anatoa simu aliyokuwa ameficha ndani ya  "chupi" baada ya kulazimishwa kufanya hivyo na wananchi wenye hasira kali....

Rajabu akilia kwa uchungu baada ya kushushiwa kipondo cha Mbwa Mwizi....


Piga............

Wananchi wakishuhudia mkanda mzima......

hatimaye kibaka huyo alitoa simu hiyo aliyokuwa amificha ndani ya "Chupi" yake.....

Wafanyakazi wa Fresh Coach Restaurant, Leon Mbisye (aliyevaa nguo ya kimasai jekundu) na mwenzake Alhadji wakifuatilia tukio la wizi, huku wakiwa wameacha kazi ya kuhudumia wateja katika mgahawa huo maarufu mjini hapa....

Kipondo kinaendelea....kwa mbali anaonekana mwandishi wa Gazeti la HABARI LEO (mwenye suti nyeusi), Arnold Swai, akishuhudia tukio zima....

Yere wiiiii...............................

Habari Zingine

0 MAOINI :

Fadhili Athumani



EastAfrica Swahili Blogger, Journalist at Mwanaspoti Kenya, Nairobi Kenya, Call: +254705246475, whatsapp:+255654724337, Email: fadhiliathumani85@gmail.com

Proudly Powered by EAMG .