EXTRA BONGO KUPAGAWISHA MKESHA KILIMANJARO MARATHON KESHO
No comments
Thursday, February 27, 2014
By
danielmjema.blogspot.com
Kiongozi wa Extra Bongo Ally Choki jukwaani |
Na Mwandishi Wetu, Moshi
WASANII mbalimbali wanatarajia kutoa burudani kesho
usiku katika Ukumbi wa Voda House mjini Moshi ikiwa ni mkesha kabla ya
kufanyika kwa mashindano ya mbio za Kilimanjaro Marathon Jumapili
zitakazoanzia katika Uwanja wa Chuo cha Ushirika.
Meneja wa Bia ya Kilimanjaro Premium Lager, George Kavishe amesema
jijini Dar es Salaam jana kuwa burudani hiyo ni moja ya hamasa kabla ya
kufanyika kwa mbio hizo.
Aliwataja wasani watakaotoa burudani katika siku ya mkesha huo wa Kilimanjaro Marathon kuwa ni Jambo Squad, The Warriors na Extra Bongo.
Aliwataja wasani watakaotoa burudani katika siku ya mkesha huo wa Kilimanjaro Marathon kuwa ni Jambo Squad, The Warriors na Extra Bongo.
“Kwa mwaka huu tumeona tufanye tofauti kwa kuweka burudani katika
siku ya mkesha kabla ya kufanyika Kilimanjaro Marathon,” alisema.
Alisema pia siku ya mashindano hayo ya Kilimanjaro Marathon
kutakuwepo na burudani kutoka kwa Joh Makini, Jambo Squad, Wakali
Dancers na FM Academia ‘Wazee wa Ngwasuma.
Mbio hizi zinaratibiwa na kwa kushirikiana na Riadha Tanzania,
Chama cha Riadha Mkoa wa Kilimanjaro na Kilimanjaro Marathon Club huku
zikidhaminiwa na Kilimanjaro Premium Lager, Vodacom Tanzania, GAPCO,
Simba Cement, KK Security, Keys Hotel, TPC Sugar, TanzaniteOne, CMC
Automobiles Ltd, Kibo Palace Hotel, RwandAir, FNB Tanzania, UNFPA na
Kilimanjaro Water.
Habari Zingine
Mjulishe Mwenzako
0 MAOINI :