LEMBELI ATAHADHARISHA KUPOTEA KWA TEMBO NA NYUMBU KUFUNGWA KWA MASHOROBA TARANGIRE

No comments
Saturday, February 8, 2014 By danielmjema.blogspot.com

Mwandishi Wetu, Manyara
 

Mwenyekiti wa Kamati ya Ardhi, Maliasili na Mazingira, James Lembeli ametahadharisha kuhusu uwezekano wa wanyama wa hifadhi ya tarangire kutoweka kutokana na njia ambazo hutumiwa na wanyama hao katika mizunguko yao kuzibwa kutokana na shuguli za kibinadamu kama vile makazi na mashamba makubwa.

Lembeli alitoa kauli hiyo juzi baada ya kupokea taarifa ya kiutendaji kutoka kwa Mhifadhi wa hifadhi ya Tarangire, Steven Koli ambaye alisema wanyama hao kwa sasa wamepungua mno kutokana na njia za mizunguko yao kuziba.

Awali akitoa taarifa ya hifadhi kwa kamati hiyo, Mhifadhi mkuu wa hifadhi ya Tarangire, Steve Koli alisema kumekuwa na idadi kubwa ya watu katika maeneo yanayozunguka hifadhi limeongeza mahitaji ya ardhi kwa ajili ya kilimo, makazi, ufugaji na shughuli zingine za binadamu.

Koli alisema ongezeko hilo limesababisha kufungwa kwa baadhi ya shoroba (wildlife corridors) ambazo ni njia za kupita wanyama, njia ambazo ni muhimu kwa ajili ya wanyama wahamao hususan Nyumbu, Pundamilia na Tembo.
Lembeli alisema wakati hifadhi hiyo inaanzishwa mwaka 1970, kulikuwa na jumla ya njia tofauti 9 lakini kutokana na njia hizo kuzibwa hadi kufikia 3 wanyama hao waikuwa ni 9 kwa sasa zimeonekana kuzibwa  na kufikia 3 tu kutokana  na aidha ujenzi wa makazi ya binadamu au mashamba makubwa.

Alisema hifadhi zinategemeana na kwa maana hiyo wanyama huzunguka kwa kutumia njia maalum, kwa mfano wanyama walioko tarangire wapo wanaotoka maeneo ya ngorongoro na wengine wanakwenda kwenye maeneo ya simanjiro ambayo iko nje kabisa ya maeneo ya simanjiro ambayo iko nje ya hifadhi.

“Sasa kuna wimbi la hizo njia za wanyama kuzibwa, aidha kwa makazi ya binadamu au mashamba makubwa hususan katika eneo hili, hali hii ni hatari kwa maisha ya hifadhi zetu hapa nchini hasa hizi za kaskazini zote,” alisema Lembeli.
 

Alisema Kama mzunguko unaowafanya wanyama wahame kutoka eneo fulani kwenda eneo lingine, kwenda kuzaa au kutafuta watoto, itakakosekana, kuna hatari ya wanyama kutotunga mimba na  matokeo yake wanyama watakuwa, watazeeka, watakufa na hakutakuwa na wanyama wengine.

“Jambo hili ni jambo ambalo kuanzia serikali za mitaa, kwenye Halmashauri za wilaya na kadhalika watambue umuhimu wa maeneo ya hifadhi za taifa, huu ndio urithi pekee ambao tunaweza kuendelea kujivunia sisi watanzania, Tanzania inajulikana duniani kote kwa uhifadhi wa wanyapori kwa watu wenye mapenzi mema wasiokuwa wagomvi, kwa hiyo tuiendeleze,

“Ombi letu na sisi katika ngazi ya bunge tutaendelea kuishauri serikali kwamba ni muhimu sheria zilizoko zinazohusu shoroba zinazingatiwa,” alisema Lembeli.


Habari Zingine

0 MAOINI :

Fadhili Athumani



EastAfrica Swahili Blogger, Journalist at Mwanaspoti Kenya, Nairobi Kenya, Call: +254705246475, whatsapp:+255654724337, Email: fadhiliathumani85@gmail.com

Proudly Powered by EAMG .