RAIS KIKWETE KUZINDUA SHUGHULI ZA BUNGE MAALUM LA KATIBA LEO
Posted in
Siasa
No comments
Friday, March 21, 2014
By
danielmjema.blogspot.com
Rais wa Tanzania Jakaya Kikwete
leo anatarajiwa kuzindua rasmi shughuli za bunge la kitaifa kuhusu
marekebisho ya katiba mjini Dodoma katika hatua itakayoanzisha rasmi
mjadala wa kitaifa kuhusu marekebisho hayo.
Suala la hotuba ya Rais Kikwete limekuwa sehemu ya mjadala katika Bunge hilo kutokana na baadhi ya wajumbe kuhoji sababu za Jaji Warioba kuwasilisha Rasimu kabla ya Rais kuzindua Bunge kwa mujibu wa kanuni.
Mjadala huo uliwafanya baadhi ya wajumbe kumzuia Jaji Warioba Jumatatu iliyopita kuwasilisha rasimu hiyo kama ilivyokuwa imepangwa.
Kikao cha maridhiano kilifanyika siku hiyohiyo usiku na kufikia mwafaka kwamba Mwenyekiti huyo wa Tume ya Mabadiliko ya Katiba awasilishe Rasimu ndiposa Rais aweze kuzindua shughuli ya kujadili rasimu hiyo kabla ya kura ya maoni.
Kikwete na ujumbe mzito
Kwa mujibu wa taarifa zilizotolewa jana na Katibu wa Bunge Maalumu la Katiba, Yahaya Khamis Hamad, Rais Kikwete atahutubia Bunge hilo kwa mujibu wa Kanuni ya 75 (1) ambapo ataambatana na ujumbe mzito wa marais
wastaafu wa pande zote za Muungano, wake wa waasisi wa taifa na mawaziri
wakuu wastaafu atakapokwenda kuzindua Bunge Maalumu la Katiba.
Hatua ya Rais kuambatana na ujumbe huo imepongezwa
na viongozi wa vyama vikuu vya upinzani nchini, Mwenyekiti wa CUF,
Profesa Ibrahim Lipumba na mwenzake wa Chadema, Freeman Mbowe.
Mbali na viongozi hao, Rais Kikwete pia
ataambatana na Rais wa Zanzibar, Dk Ali Mohamed Shein na Makamu wa Rais,
Dk Mohamed Gharib Bilal na Makamu wa Kwanza wa Rais wa Zanzibar, Seif
Sharif Hamad.
Wanaotarajiwa kuwamo katika msafara huo ni Rais wa
pili wa Tanzania, Ali Hassan Mwinyi, Rais wa tatu, Benjamin Mkapa na
marais wastaafu wa Zanzibar, Dk Salmin Amour na Amani Abeid Karume, Mama
Maria Nyerere na Mama Fatma Karume.
Mwenyekiti wa Bunge maalum la Katiba-Samwel Sitta |
Mawaziri wakuu wengine ni Cleopa Msuya, John
Malecela, Dk Salim Ahmed Salim, Frederick Sumaye pamoja na Edward
Lowassa na Mizengo Pinda ambao ni wajumbe wa bunge hilo.
Wengine walioalikwa ni mabalozi wa nchi
mbalimbali, wawakilishi wa mashirika ya kimataifa, viongozi wa dini,
vyama vya wafanyakazi, vyama vya siasa, wafugaji, wakulima, wavuvi na
wawakilishi wa sekta binafsi.
Rais Kikwete atapokewa katika Viwanja vya Bunge na
Mwenyekiti wa Bunge Maalumu la Katiba, Samuel Sitta na baadaye kukagua
gwaride maalumu kabla ya kuhutubia Bunge kuanzia saa 10:00 jioni.
Baadhi ya wajumbe wa bunge hilo |
Kwa mujibu wa ratiba iliyotolewa jana, baada ya
Rais kuhutubia saa 11:35 jioni, aliyekuwa mwenyekiti wa muda wa bunge
hilo, Pandu Ameir Kificho atatoa neno la shukurani kabla ya Rais kupiga
picha za kumbukumbu na wajumbe wa Bunge hilo.
Suala la hotuba ya Rais Kikwete limekuwa sehemu ya
mjadala katika Bunge hilo kutokana na baadhi ya wajumbe kuhoji sababu
za Jaji Warioba kuwasilisha Rasimu kabla ya Rais kuzindua Bunge kwa
mujibu wa kanuni.
Mjadala huo uliwafanya baadhi ya wajumbe kumzuia
Jaji Warioba Jumatatu iliyopita kuwasilisha rasimu hiyo kama ilivyokuwa
imepangwa hadi kilipofanyika kikao cha maridhiano siku hiyohiyo usiku na
kufikia mwafaka kwamba Mwenyekiti huyo wa Tume ya Mabadiliko ya Katiba
awasilishe Rasimu Jumanne, Machi 18 mwaka huu, na Rais ahutubie leo.
Habari Zingine
Mjulishe Mwenzako
0 MAOINI :