BURUNDI: KABURI LA ALAIKI LAGUNDULIKA MUTAKURA KASKAZINI MWA BUNJUMBURA
                      Posted in 
                      
afrika mashariki
                            No comments
                          
Monday, February 29, 2016
                      By 
                      danielmjema.blogspot.com
Maafisa wa polisi na utawala wa mji 
mkuu wa Bujumbura Burundi wamegundua kaburi la halaiki linaloshukiwa 
kuwa na takriban miili 30. Mwandishi wa BBC aliyeko huko Prime 
Ndikumagenge anasema kuwa miili 3 na fuvu la kichwa ilipatikana katika 
eneo la Mutakura  Kaskazini mwa Bujumbura.
Kitongoji hicho cha 
Mutakura ni moja ya ile iliyosheheni wafuasi wa upinzani ambao 
walijitokeza barabarani wakiandamana kupinga kauli ya rais Pierre 
Nkurunziza kuwania muhula wa tatu uongozini. Nkurunziza alitangaza
 nia ya kuwania muhula  wa tatu mwezi Aprili mwaka uliopita kinyume cha 
katiba akidai kuwa mhula wa kwanza hakuchaguliwa na umma.
Wapinzani wake hata hivyo wanadai kuwa alikiuka katiba ya taifa. Meya wa mji wa  Bujumbura Freddy Mbonimpa  anasema walipokea habari hiyo kutoka kwa ''wahuni waliojisalimisha kwa utawala''.
Haikuelezwa kwa hakika waliuawa lini au na nani na nani aliyewazika pahala hapo. Meya huyo hata hivyo alidai kuwa waliopatikana wameuawa walikuwa ni wafuasi wa rais Nkurunziza.
Kuwepo kwa makaburi ya halaiki kuligunduliwa kwanza na kundi 
linalopigania haki za kibinadamu  la Amnesty International mwezi 
Januari. Ripoti hiyo ya kundi la kutetea haki za binadamu la 
lilichapishwa  tarehe 11 Desemba mwaka uliopita siku moja baada ya 
serikali kukiri kuwa wamewaua watu 79 na kupoteza maafisa 8 wa  polisi.
Meya huyo leo amekiri kuwa utawala wake ulizika miili ya watu 58 katika makaburi ya halaiki katika makaburi yanayofahamika. Umoja
 wa Mataifa unasisitiza kuwa zaidi ya watu  430 waliuawa nchini Burundi 
tangu kauli ya rais Nkurunziza kubainika mwezi Aprili.
SOURCE: BBC SWAHILI
SOURCE: BBC SWAHILI
Habari Zingine
Mjulishe Mwenzako


0 MAOINI :