KENYA: SIMBA WAWILI WAONEKANA BARABARANI NAIROBI
Posted in
afrika mashariki
No comments
Monday, February 29, 2016
By
danielmjema.blogspot.com
Simba wawili wameonekana katika
barabara moja ya mji mkuu wa Kenya, Nairobi wiki moja tu baada ya simba
wengine kutoroka kutoka mbuga ya taifa ya Nairobi.
Simba hao walionekana na polisi wa trafiki, waliokuwa wakipiga doria katika barabara ya Southern Bypass, mwendo wa saa nne asubuhi, shirika la huduma kwa wanyamapori (KWS) limesema kupitia taarifa.
Wanyama hao walionekana wakitembea karibu na ua unaozunguka msitu wa barabara ya Ngong, karibu na kituo cha idara ya misitu ya Kenya (KFS).
Polisi hao waliwapasha habari maafisa wa KWS ambao wameanza operesheni ya kuwatafuta wanyama hao.
Siku kumi zilizopita, simba sita waliotoroka kutoka mbuga ya taifa ya Nairobi walionekana katika eneo lenye watu wengi la Langata.
Baadaye, simba jike na shibli wake walipatikana na wakarejeshwa kwenye mbuga hiyo. Simba hao wengine inaaminika walirejea wenyewe kwenye mbuga.
CHANZO: BBC SWAHILI
Habari Zingine
- WENGI WALIVYOJITOKEZA KUMUAGA MWANA TBN JENNIFER LIVIGHA (CHINGA ONE) HOSPITALI YA AMANA JIJINI DAR
- Wachimbaji mgodi 15 waliokwama ardhini waokolewa nchini Tanzania
- Al-Shabab washambulia kambi ya majeshi ya Kenya nchini Somalia
- UHURU WA HABARI SIO KUIANGALIA TU SERIKALI - MWAKYEMBE
- JUKWAA LA WAHARIRI TANZANIA LATANGAZA KUSUSIA KUANDIKA HABARI ZA MKUU WA MKOA WA DAR
Mjulishe Mwenzako
0 MAOINI :