Tetesi za Soka Ulaya Jumamosi 05.05.2018

Posted in
No comments
Saturday, May 5, 2018 By danielmjema.blogspot.com

Meneja wa Manchester United, Jose Mourinho anamtolea macho mshambuliaji wa Napoli, Dries Mertens. Mchezaji huyo mwenye miaka 30 amefunga magoli 45 katika kipindi cha misimu miwili iliyopita kwenye ligi ya Serie A.(Sun).
Kiungo mshambuliaji raia wa Algeria, Riyad Mahrez ametupilia mbali ombi la kuondoka Leicester lakini Mahrez mwenye miaka 27 bado hajatulia katika timu yake ya Leicester. (Sky Sports)
Mrithi wa Arsene Wenger atapatiwa bajeti ya usajili kiasi cha pauni milioni 200, huku Kocha wa Juventus Massimiliano Allegri akipigiwa upatu kushika mikoba ya Wenger.
Hata hivyo, Arsenal na Chelsea wanamtaka Kocha wa Monaco,Leonardo Jardim, ambaye anatarajiwa kuiacha klabu hiyo mwishoni mwa msimu.(Sun)
AC Milan wanataka kumchukua kiungo wa kati wa Manchester United, Marouane Fellaini (30) raia wa Ubelgiji. Mchezaji huyo atamaliza mkataba wake mwishoni mwa mwezi June.(Corriere dello Sport via Talksport)
Kiungo mshambuliaji wa Everton, Kevin Mirallas amevunjiwa mkataba na klabu ya Olympiakos. Amefunga magoli mawili katika michezo 13 ya ligi kuu ya Uturuki. (Liverpool Echo)
Mabingwa wa ligi daraja la kwanza Wolves wanataka kumsajili mlinda mlango wa Southampton,Alex McCarthy (Mirror)
Kiungo wa kati wa Arsenal Santi Cazorla amesema hajapatiwa mkataba mpya, mkataba anaoutumikia sasa utaisha kipindi cha majira ya joto(ESPN)
Kiungo mshambuliaji wa Manchester City Yaya Toure anataka kuendelea kucheza ligi kuu .Toure ataondoka City mwishoni mwa msimu baada ya miaka minane Etihad.(Manchester Evening News)
Kocha wa Palace, Roy Hodgson amesema ''hana mpango'' wa kustaafu.Hodgson, mwenye miaka 70, amebakisha mwaka mmoja kumaliza mkataba wake. (Evening Standard)

Peter Crouch amesema ataangalia mustakabali wake iwapo Stoke itashuka daraja msimu huu. Mshambuliaji huyo mwenye miaka 37 alisaini mkataba wa mwaka mmoja mwezi Novemba. (Sky Sports)
Mlinzi wa kati Aston Villa John Terry amesema ataendelea kubaki Villa Park kwa msimu mwingine iwapo watapanda ligi kuu. Kapteni huyo wa zamani wa timu ya taifa ya England alitia saini mkataba wa mwaka mmoja majira ya joto mwaka hana baada ya kuondoka Chelsea. (Manchester Evening News)
Kocha mpya wa Rangers, Steven Gerrard anamnyemelea aliyekuwa mchezaji mwenzake kwenye kikosi cha Liverpool, Martin Skrtel kuwa mmoja wa wachezaji wa kwanza kusajiliwa . Skrtel anaichezea klabu ya Fenerbahce ya Uturuki.(Daily Record)
Mlinda mlango wa Watford, Orestis Karnezis anataka kurejea nyumbani, Ugiriki, Mchezaji huyo (30) amesema anapenda kuichezea Olympiakos.(Watford Observer)

Habari Zingine

0 MAOINI :

Fadhili Athumani



EastAfrica Swahili Blogger, Journalist at Mwanaspoti Kenya, Nairobi Kenya, Call: +254705246475, whatsapp:+255654724337, Email: fadhiliathumani85@gmail.com

Proudly Powered by EAMG .