DORTMUND YAITANDIKA BAYERN 4-2 FAINALI YA GERMAN SUPER CUP

Posted in
No comments
Sunday, July 28, 2013 By danielmjema.blogspot.com

BORUSSIA DORTMUND Jana Usiku kwenye Uwanja wao wa Nyumbani Signal Iduna Park walimaliza ule utawala wa hivi karibuni wa Bayern Munich kwenye Soka la German baada ya kuibonda 4-2 na kutwaa German Super Cup.

MAGOLI:
BV Borussia Dortmund 4
-Marco Reus Dakika ya 6 -Daniel Van Buyten 56 [Kajifunga mwenyewe] -Ilkay Gundogan 57
-Marco Reus 86 
Bayern Munich 2
-Arjen Robben Dakika ya 54 & 64

Marco Reus ndie aliefungua na kufunga kitabu cha Magoli ya Borussia Dortmund kwa kufunga Bao la kwanza na la mwisho.Arjen Robben alijitahidi kuiletea Bayern ushindi kwa kwanza kusawazisha na kuifanya gemu iwe 1-1 na baadae kupunguza Mabao kuwa 3-2 lakini hiyo haikusaidia kwani Dortmund walichachamaa na kupiga Bao la 4 kumuonyesha Kocha mpya wa Bayern, Pep Guardiola kuwa kwenye Bundesliga kazi ipo.

AJAX YAIFUNGA ALKMAAR, YATWAA SUPER CUP

HUKO Holland, Siem de Jong alifunga Bao la ushindi katika Dakika za Nyongeza 30 na kuipa Ajax Amsterdam ushindi wa Bao 3-2 dhidi ya AZ Alkmaar baada ya kutoka nyuma Bao 2-0 na kutwaa Holland Super Cup, rasmi kama Johan Cruijff Schaal, katika Mechi iliyochezwa Jijini Amsterdam hapo Jana.

Hadi Mapumziko Bao zilikuwa 0-0 na Kipindi cha Pili AZ walipiga Bao mbili kupitia Johann Berg Gudmundsson katika Dakika za 51 na 67.

Ajax walisawazisha katika Dakika za 69 na 75 kwa Bao za Christian Eriksen na Kolbeinn Sigthorsson.
Bao la ushindi la Ajax, lililofungwa na Siem de Jong, lilipatikana katika Dakika ya 103.

Habari Zingine

0 MAOINI :

Fadhili Athumani



EastAfrica Swahili Blogger, Journalist at Mwanaspoti Kenya, Nairobi Kenya, Call: +254705246475, whatsapp:+255654724337, Email: fadhiliathumani85@gmail.com

Proudly Powered by EAMG .