TAIFA STARS KUUMANA NA THE CRANES LEO; UWANJA WA NAMBOOLE-KAMPALA

Posted in
No comments
Saturday, July 27, 2013 By danielmjema.blogspot.com

LEO, huko Kampala, Wenyeji Uganda, ambao walishinda 1-0 katika Mechi ya kwanza Jijini Dar es Salaam, wanarudiana na Tanzania kwenye Mechi ya CHAN kweye Uwanja wa Mandela, Namboole, ambao hawajafungwa tangu Mwaka 2004.

Mshindi wa Mechi hii atatinga Fainali za CHAN, Mashindano maalum ya CAF yanayoshirikisha Wachezaji wanaocheza Ligi za ndani ya Nchi zao tu, zitakazochezwa huko Afrika Kusini kuanzia Tarehe 10 Januari 2014.

Wakati Uganda, ambao waliifunga Tanzania Bao 1-0 kwa Bao la Dakika ya 46 la Denis Iguma katika Mechi ya kwanza Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam Wiki mbili zilizopita, wanahitaji sare tu, Tanzania ni lazima washinde Mechi hii.
Kwa kutambua hilo, Kocha wa Tanzania, Kim Poulsen, hapo Jana huko Kampala alitamka: “Unapocheza mechi za aina hii za nyumbani na ugenini, huku mwenyeji akiwa anaongoza mabao yana maana kubwa katika mechi. Mabao yanabadili mchezo na pia wachezaji kifikra. Hivyo tuko hapa kwa ajili ya kufunga, ni lazima tufunge ili tuweze kuendelea na mashindano. Lakini ngome yetu nayo ni lazima iwe makini ili kutoruhusu bao.”
Lakini Uganda, chini ya Kocha kutoka Serbia, Milutin Sedrojevic, na Nahodha wao Hassan Wasswa Mawanda, ni Timu hatari na wenyewe wameshaahidi kuidhibiti Taifa Stars.
Katika Mechi ya leo, Uganda itawakosa Mastraika wao wawili waliocheza Dar es Salaam, Patrick Edema na Tonny Odur, kwani Edema ameenda Portugal kwa majaribio na Odur ni majeruhi lakini wataongezewa nguvu kwa kurudi Uwanjani Beki wao wa kushoto Habib Kavuma alieikosa Mechi ya kwanza kwa kuwa na Kadi.

UGANDA CRANES (Mfumo 4-2-1-3):

Hamuza Muwonge, Nicolas Wadada - Savio Kabugo - Richard Kasagga – Habibu Kavuma, Hassan Wasswa-Dennis Iguma, Joseph Mpande Saidi Kyeyune–Frank Kalanda – Brian Majwega

TAIFA STARS: (Mfumo: 4-3-3):
Juma Kaseja, Erasto Nyoni - Aggrey Morris  - Kevin Yondon- David Luhende, Frank Damayo-Athumani Iddi-Amri Kiemba, Mrisho Ngassa-John Bocco - Salum Abubaker

REFA: Abduol Kanoso Ohabee [Madagascar]

Habari Zingine

0 MAOINI :

Fadhili Athumani



EastAfrica Swahili Blogger, Journalist at Mwanaspoti Kenya, Nairobi Kenya, Call: +254705246475, whatsapp:+255654724337, Email: fadhiliathumani85@gmail.com

Proudly Powered by EAMG .