KANISA KATOLIKI YAKANA RIPOTI YA AU KUHUSU UDHALILISHAJI WA MAPADRI NA MAASKOFU DHIDI YA WATOTO
Posted in
Kimataifa
No comments
Thursday, February 6, 2014
By
danielmjema.blogspot.com
Uongozi wa kanisa katoliki duniani mjini Vatican umelaani
vikali ripoti ya Umoja wa Mataifa iliyotolewa hapo jana ikilituhumu
kanisa hilo kuwalinda mapadri na maaskofu ambao wanatuhumiwa kuhusika na
vitendo vya udhalilishaji dhidi ya watoto.
![](https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEiuajLeRmT4YLjJQERei7M_Ih6cvc5BMV1mkUKiETkIq2MHK4Uwi4qwFV-bZZlxvpYn0e_rU1j7rtoJJiPlqqX3iu3S59wYFu53OFkmQ8RSugVone9u6AM-QbuQht8ms2OAmpu43f168tg/s1600/POPE.jpg)
POPE FRANCIS
![](https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEiuajLeRmT4YLjJQERei7M_Ih6cvc5BMV1mkUKiETkIq2MHK4Uwi4qwFV-bZZlxvpYn0e_rU1j7rtoJJiPlqqX3iu3S59wYFu53OFkmQ8RSugVone9u6AM-QbuQht8ms2OAmpu43f168tg/s1600/POPE.jpg)
Mara baada ya kutolewa kwa ripoti ya UN inayokemea sera za kanisa hilo pamoja na viongozi hao wa kidini kulindwa na uongozi wa juu wa kamati ya Papa, bado kanisa hilo limedai ripoti hiyo ni ya uongo na inayopandikiza chuki kwa waumini wake kwa kuwa kwa sehemu kubwa imetekeleza mapendekezo mengi ambayo yametolewa na tume ya Umoja wa mataifa iliyokuwa ikichunguza tuhuma za udhalilishaji wa watoto dhidi ya kanisa hilo.
Wakati wamahojiano yao na kamati maalumu ya Umoja wa Mataifa majuma
kadhaa yaliyopita, viongozi wa kanisa hilo walikiri kuwepo kwa vitendo
hivyo na kwamba kesi nyingi wamezishughulikia kama kanisa na ni masuala
yanayohusu imani zaidi.
Ripoti ya UN inalitaka kanisa hilo kuwakabidhi mapadri na maaskofu
waliohusika na vitendo hivyo kwa vyombo vya usalama, pamoja na kuondoa
ukiritimba wa upatikanaji wa taarifa muhimu za ndani ya kanisa hilo
kuhusu matukio kama haya.
CHANZO:RFI/SWAHILI
Habari Zingine
Mjulishe Mwenzako
0 MAOINI :