"CONTE ANA KIBARUA CHA KUISUKA UPYA CHELSEA"-HIDDINK

Posted in
No comments
Sunday, April 10, 2016 By danielmjema.blogspot.com

Muitaliano Antonio Conte anakabiliwa na kazi kubwa wakati akichukua mikoba katika klabu ya Cheslea msimu ujao. Hayo ni maneno ya kaimu kocha wa Guus Hiddink. 

Kocha wa zamani wa Jubentus Conte ametangazwa kuwa mrithi wa Hiddink na ataanza enzi mpya uwanjani Stamford Bridge baada ya kuiongoza Italia katika dimba la Mataifa ya Ulaya nchini Ufaransa mwezi Juni.

Kazi yake itakuwa ni kuwarejesha mabingwa hao wa msimu uliopita kileleni mwa Premier League baada ya kuwa na msimu mbovu. Hiddink anahisi kuwa kikosi hicho cha Chelsea inakosa wachezaji ambao wanaweza kutegemewa katika kutoa mwongozo wa mafanikio kama ilivyokuwa katika muongo mmoja uliopita.

Hiddink alikutana na Conte Jumatatu wiki hii baada ya kocha huyo mtarajiwa kuzuru uwanja wa mazoezi wa Chelsea ili kujifahamisha na mazingira yake mapya.

Habari Zingine

0 MAOINI :

Fadhili Athumani



EastAfrica Swahili Blogger, Journalist at Mwanaspoti Kenya, Nairobi Kenya, Call: +254705246475, whatsapp:+255654724337, Email: fadhiliathumani85@gmail.com

Proudly Powered by EAMG .