Ibrahimovic anakaribia kusaini Manchester United

Posted in
No comments
Saturday, June 4, 2016 By danielmjema.blogspot.com

Timu ya Manchester United inatarajiwa kukamilisha usajili wa mchezaji wa Swedan, Zlatan Ibrahimovic kabla ya kuanza kwa michuano ya Uero Juni 10 mwaka huu.

Sky Sports imeripoti kuwa kaimu mtendaji mkuu wa Manchester United, Ed Woodward na wakala wa mchezaji huyo wanakamilisha makubaliano ya hatua za mwisho kwa ajili ya kumsajili mchezaji huyo kwa mkataba wa mwaka mmoja ambaye kocha mpya wa timu hiyo, Jose Mourinho amepanga kumtangaza Ibrahimovic kama ndiyo usajili wake wa kwanza ndani ya timu hiyo.


Ibrahimovic ni mchezaji huru kwa sasa baada ya kumalizika kwa mkataba wake na timu yake ya zamani PSG aliyeichezea kwa zaiodi ya misimu mitatu kwa mafanikio makubwa zaidi.

Habari Zingine

0 MAOINI :

Fadhili Athumani



EastAfrica Swahili Blogger, Journalist at Mwanaspoti Kenya, Nairobi Kenya, Call: +254705246475, whatsapp:+255654724337, Email: fadhiliathumani85@gmail.com

Proudly Powered by EAMG .